July 12, 2018

Dkt. Kalemani ameendelea na uzinduzi Miradi ya Umeme Vijijini Mkoani Tabora


Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani, ameendelea na ziara ya uzinduzi wa Miradi ya Umeme Vijijini Awamu ya Tatu katika Wilaya za Kaliua, Sikonge na Uyui Mkoani Tabora.

Dkt. Kalemani amezindua katika Vijiji vya Ghuliyankulu, Mbeta, Uyowa, Mkindo na Mwongozo vilivyopo Wilaya ya Kaliua.

Vijiji vingine ni Kisanga na Kanyamsenga katika Wilaya ya Sikonge.

Mheshimiwa Waziri ataendelea na ziara kesho ambapo anatarajiwa kutembelea kijiji cha Mbuyuni kilichopo Wilaya ya Uyui.


No comments:

Post a Comment