July 11, 2018

TANESCO Rukwa, NMB watembelea Gereza la Molo

Wafanyakazi wa Shirika la Usambazaji umeme ( TANESCO) Mkoa wa Rukwa wakishirikiana na Benki ya NMB wamewatembelea Maafisa wa Magereza wa Gereza la Molo lililopo Mkoani Rukwa na kutoa elimu inayohusu taratibu za kuunganishiwa huduma ya umeme kupitia Mradi wa REA awamu ya Tatu.

 katika ziara hiyo, Wateja wapatao 96 ambao ni  Wafanyakazi wa Gereza hilo waliweza  kuunganishiwa huduma ya umeme kupitia mradi wa umeme vijijini  awamu ya Tatu. 

Mbali na kuunganishiwa huduma ya umeme Maafisa hao wa Magereza walipatiwa mafunzo juu ya namna ya kupata huduma, matumizi sahihi ya kutumia nishati ya umeme, usalama juu ya umeme, ulinzi wa miundombinu ya umeme na umuhimu wa kutumia umeme ili kuchochea maendeleo Nchi.

Baadhi ya Maafisa wa gereza la Molo wakisikiliza kwa makini elimu na taratibu za kupata umeme kupitia mradi wa umeme vijijini REA 3
              
Mkuu wa Gereza la Mollo ACP J.L  Mwamgunda,Afisa Mahusiano na Huduma kwa Wateja Ndg Lucas C. Kusare na Afisa wa upimaji wakisikiliza maswali kutoka kwa Maofisa wa gereza hilo.

Afisa wa Masoko na Huduma kwa Wateja NMB benki tawi la Sumbawanga akitoa maelezo ya namna ambavyo wateja wa TANESCO wanavyoweza kutumia mfumo wa Benki yao ili kufanya malipo ya huduma mbalimbali za umeme.
Afisa Huduma na Mahusiano kwa Wateja TANESCO Mkoa wa Rukwa akiwafafanulia maofisa wa Gereza la Molo juu ya utaratibu wa kupata huduma ya umeme kupitia mradi wa umeme wa REA 3

Afisa wa Gereza akiulizia utaratibu wa namna ya kupata huduma za umeme kupitia Mpango wa REA 3






No comments:

Post a Comment