July 18, 2020

Mradi wa Julius Nyerere hatua zote 8 zakamilika

Mafundi wakiwa wamebeba nondo wakati kazi ya ujenzi wa njia ya ardhi ya kuchepusha maji (dirvesion tunnel) ikiendelea.

HATUA zote nane (8) za utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa bwawa la kufua umeme wa maji la Julius Nyerere (JNHPP-MW2115) kwenye bonde la mto Rufiji unaendelea kwa kasi inayohitajika, Mhandisi mkazi wa mradi huo Eng. Mushubila Kamuhabwa amewaambia waandishi wa habari kwenye eneo la mradi Julai 17, 2020.

Eng. Kamuhabwa ametaja hatua hizo kuwa ni ujenzi wa njia kubwa ya ardhini ya mchepuko wa maji (diversion tunnel), sehemu ya kufua umeme (power house), ukuta utakaotengeneza bwawa, eneo la kupokelea umeme unapozalishwa (Switch yard), power intake, barabara na madaraja, saddle dams nne na kuchakata mawe yanayotumika kutengeneza zege na mahitaji mengine.

“Mradi huu wa JNHPP una miradi mingi ndani yake na yote iko katika hatua mbalimbali na hatua hizo kama nilivyozitaja kwa pamoja ndiyo zinajenga mradi mmoja wa Julius Nyerere Hydro Power Project Megawati 2115 katika hilo ujenzi unaendelea katika maeneo yote hayo, mafundi wako kazini na wanaendelea na ujenzi kwa kasi kubwa kama inavyohitajika.” Alisema Eng. Kamuhabwa.

Alisema jambo la kufurahisha tayari mradi umeanza kuchangamsha uchumi wa nchi na kutolea mfano wakati wakiweka zege kwenye njia ya kuchepusha maji (diversion tunnel, zaidi ya tani 200 za nondo zimetumika hii inafaidisha viwanda vyetu hapa nchini lakini pia wananchi wanaokaa vijiji vinavyozunguka eneo la mradi wanafaidika kwa namna mbalimbali ikiwwemo miundombinu wezeshi kama vile umeme unaotoka Morogoro kuja hapa umepitia kwenye vijiji kadhaa natayari baadhi yao wameanza kufaidika na umeme huo.” Alisema na kuongeza…Lingine zaidi ya vijana wa Kitanzania wapatao 4,000 kutoka maeneo mbalimbali nchini hususan yale yanayozunguka eneo la mradi wameajiriwa na wanashiriki katika mradi kwa ari kubwa.

“Tunatarajia idadi hiyo ya ajira ikaongezeka hadi kufikia watu 6,000 mradi utakapofikia hatua ya juu peak.” Alisema Eng. Kamuhabwa.

Kwa upande wao baadhi ya wanakijiji wa Kisaki kilomita 60 kutoka eneo la mradi wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Magufuli kwa kuwaletea mradi huo kwani tayari manufaa yake wameanza kuyaona.

“Kisaki inakuja juu, tuna uhakika mradi ukimalizika Kisaki itakuwa kama Morogoro, kwa sasa biashara inakuwa kwa kasi sana tofauti na hapo awali, mfano mchele tunauza kwa kilo shilingi 1,600/= tofauti na hapo awali tulikuwa tunauza shilingi 500/= bei ya juu kabisa shilingi 1,000/=, watu wameongezeka sana.” Alisema mwanakijiji wa Kisaki Ali Matumbo na kuongeza…umeme nao tayari umefika kijijini kwetu, shule imepata umeme kwa hivyo tunafuraha sana kwa ujio wa mradi huu na tunampongeza sana Rais wetu Magufuli.

Naye mwanakijiji mwingine Bi. Asha Said alisema, anauhakika hata barabara nzuri itajengwa kutokana na mradi huo na anafurahi kuona wageni wengi wanafika Kisaki na hivyo biashara zao zimechangamka.

Naye mwanakijiji mwingine Hassan Mohammed Ngozi alisema, anayo matumaini makubwa kwa hali anavyoiona hivi sasa hapo Kisaki, mradi utakapokamilika watakuwa na Kisaki mpya.
“Kwetu sisi ongezeko la watu hapa Kisaki limekuwa na faida kubwa………..watu wakienda kufanya kazi huko kwenye mradi wanakuja hapa kijijini wananunua bidhaa zetu na sisi tunapata pesa haya ni manufaa makubwa kwetu.” Alisema Bw. Ngozi.
Mhandisi Mkazi wa Mradi wa Julius Nyerere, Mhandisi Mushubila Kamuhabwa akizungumza na Waandishi wa Habari eneo la Mradi.

MAshine zikichoronga miamba ya ardhi ili kutengeneza njia ya kuweka baruti kwa ajili ya kulipua miamba hivyo kuhamisha milima









July 14, 2020

Utekelezaji wa Miradi ya Kimkakati



Miaka mitano imetimia Serikali  ya Awamu ya Tano ikiacha alama Sekta ya Nishati ambapo utekelezaji wa mradi Mkubwa wa kimkakati wa kufua umeme wa maji wa Julius Nyerere MW 2115 unaendelea kwa kasi.

Aidha, katika mradi wa Julius  Nyerere ujenzi wa Kituo cha Kupokea na Kusambaza Umeme (Switch yard) upo katika maandalizi ya awali ambayo ni kusafisha eneo na kufanya utafiti wa udongo yamekamilika ambayo yalianza Oktoba 2019 na Mei 2020 yamekamilika kwa kulingana na mpango kazi ulivyo.

"Utafiti wa miamba na udongo umeshafanyika pia shughuli za kusafisha eneo hilo", alisema Mhandisi Eliaza Wangwe, Mtaalamu wa miamba na udongo kwenye mradi wa Julius Nyerere.

eneo la kituo cha kupokea umeme lina ukubwa wa mita za mraba 58,075 na kituo kipo umbali wa mita 450 kutoka jengo la kuendeshea mitambo ya kufua umeme.

Zabuni ya ujenzi wa Njia Kuu ya msongo wa kilovolti 400 itakayosafirisha umeme kutoka kwenye kituo hiki kuingia kwenye gridi ya Taifa imeshatangazwa.

Aidha, utekelezaji wa maeneo mengine unaendelea na upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.