April 30, 2017

MKUU WA MKOA WA PWANI MHANDISI NDIKIRI AISHUKURU TANESCO KWA MSAADA WA VIFAA VYA USAFI

 Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikiri, (kulia), akipeana mikono na Kaimu Meenja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), Bi. Leila Muhaji, wakati akipokea msada wa vifaa vya kufanyia usafi kwa ajili ya kituo cha Afya Mkoani mjini Kibaha Aprili 29, 2017.
 NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
MKUU wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikiro, ameishukuru TANESCO kwa msaada wake wa vifaa vya kufanyia usafi kwa ajili ya Kituo cha Afya Mkoani Mjini Kibaha.
Mhandisi Ndikiro alisema, hatua hiyo yaTANESCO ni ushahidi tosha wa kuunga mkono jitihada za serikali za kuhakikisha wananchi wanapatiwa huduma afya katika mazingira ya usafi.
"Niseme tu mlichokifanya ni kitu kizuri sana, na ningeshauri taasisi nyingine za umma na binafsi, kutoa sehemu ya faida wanayopata kutokana na shughuli zao na kurudisha kwa umma kwa njia ya kusaidia shughuli za kijamii kama hii ya usafi." Alisema.
Naye Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), Bi Leila Muhaji alisema, TANESCO  kama mtoa huduma ya umeme kwa Wananchi na ikitambua kuwa wananchi ndio wateja wake wakubwa, pia imeona ni busara kusaidia serikali katika kuhakikisha mazingira yanayowazunguka kama vile kituo hiki cha afya yanakuwa safi." Alisema.
Bi. Leila pia alisema, TANESCO imetoa vifaa hivyo ili kuunga mkono juhudi za serikali za kuhamasisha umma kufanya usafi wa jumla kila mwisho wa wiki. "Tumeungana nanyi leo Jumamosi ambayo ni siku ya usafi, ili tufanye usafi pamoja kwenye kituo chetu hiki cha afya, kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, napenda muwashukuru sana na mpokee msada wetu huu mdogo ambao nina hakika utasaidia kwa sehemu fulani katika kuweka mazingira ya hospitali yawe safi." alsiema
Awali Mkuu wa Mkoa Mhandisi Ndikiro, aliwaongoza watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha, wafanyakazi wa TANESCO Mkoa wa Pwani na wachache kutoka makao makuu katika zoezi la kufanya usafi wa mazingira kwa kufyeka nyasi kuzunguka mazingira ya kituo hicho cha afya.
 Mhandisi Ndikiro, akiwa na Mganga Mkuu wa Mji wa Kibaha, akitoa hotuba yake
 Bi leila Muhaji, (katikati), akitoa hotuba yake, Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikiro, na Meneja Rasilimali watu TANESCO mkoa wa Pwani, Bi.Nisile Mwakalinga
 Wafanyakazi wa TANESCO mkoa wa Pwani
 Mhandisi Ndikiro akimshukuru Bi.Nisile, huku Bi. Leila (wapili kushoto) na Bi Salama Juma, ambaye ni Afisa Uhusiano TANESCO
 Wafanyakazi hawa wa TANESCO wakiwa wamebeba sehemu ya vifaa hivyo
 Mhandisi Ndikiro, (kulia) na Bi. Leila Muhaji wakifyeka majani kwenye eneo la Kituo hicho cha Afya
Wafanyakazi wa TANESCO wakifagia mazingira kuzunguka kituo hicho
 Mganga Mkuu wa Mji wa Kibaha, akifafanua baadhio ya mambo kwa waandishi wa habari
 Watumishi wa Halmashauri ya mji wa Kibaha, wakifyeka nyasi
 Baadhi ya wafanyakazi wa TANESCO
 Baadhi ya wafanyakazi wa TANESCO
 Mhandisi Ndikiro akiwa amenyanyua baadhi ya vifaa alivyokabidhiwa
 Watumishi wa kituo hicho cha afya wakikusanya sehemu ya vifaa hivyo
Mtumishi wa kituo cha Afya cha Mkoani mjini Kibaha, akwia amebeba sehemu ya vifaa hivyo

TANESCO yaibuka kidedea katika maonesho ya maonesho ya wakala wa Afya na Usalama Mahali pa Kazi (OSHA)





Na Magreth Subi,Moshi
Shirika la umeme Nchini Tanzania (TANESO) limeibuka kidedea katika maonesho ya wakala wa Afya na Usalama Mahali pa Kazi (OSHA) ambayo yamefikia kilele chake Aprili 28, 2017 Mjini Moshi.

 Mgeni Rasmi katika maonesho hayo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama, alitoa pongeza kwa TANESCO kwa Huduma nzuri inayotolewa katika kuhudumia jamii na kuwataka Wafanyakazi kuwa na ari siku zote pamoja na changamoto wanazokutana nazo kwani changamoto ndio chachu ya maendeleo kuelekea Nchi ya Viwanda kama kauli mbiu ya Mhe. Rais inavyo sema.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mhagama alitoa shukurani kwa washiriki na kutangaza washindi katika Nyanja mbali mbali na TANESCO kuibuka mshindi wa kwanza wa masuala ya Afya na Usalama kazini mahala pa Kazi katika Sekta ya Huduma kwa Wateja.

Kwa upande wake, Afisa Mkuu kitengo cha Afya na Usalama Kazini Bw. Fred Kayega alitoa maelezo ya vifaa mbalimbali vya vinavyotumiwa na Wafanyakazi kujikinga na ajali pahala pa kazi kwa Mhe. Mhagama alipotembelea banda la TANESCO kabla maonesho hayo hayajafikia hitimisho.

Baadhi ya Wafanyakazi wa TANESCO Makao Makuu, pamoja na Wafanyakazi wa Mkoani Kilimanjaro, walifurahia ushindi huo kwani utazidi kuongeza hari kwa Wafanyakazi na kufanya vizuri Zaidi katika utendaji wa Kazi.




April 27, 2017

TANESCO yaelimisha Jamii Siku ya Maadhimisho Ya Osha Mkoani Moshi






Na Magreth Subi, Moshi
Maadhimisho ya Siku ya Wakala wa Afya na Usalama Mahali pa Kazi (OSHA) Duniani ambayo hufanyika Aprili 28 ya kila Mwaka yanaendelea Mjini Moshi.
Maadhimisho hayo yenye kaulimbiu “Ongeza wigo wa ukusanyaji na utumiaji wa takwimu za usalama na Afya”  yameanza Aprili 24, 2017 yakijumuisha Taasisi mbalimbali za Serikali na binafsi, ambayo baadhi ni TANESCO, Acacia, Geita Gold Mine,  SSRA, Breweries na Mashirika mengine mengi.
TANESCO imeshiriki vyema chini ya Mameneja wakishirikiana na Maafisa wao kutoka Makao Makuu Mkoa wa Kilimanjaro.
Kaimu Meneja Masoko kutoka Makao Makuu, Bw. Musa Chowo alielezea kifaa cha umeme tayari kwa Wateja waliotembelea banda la TANESCO na kufurahishwa na Huduma inayotolewa pamoja na elimu waliyopatiwa.
Aidha, alielezea kifaaa cha umeme tayari  kinavyopunguza gharama hususani kwa wateja wa maeneo ya Vijijini.
 “Gharama za kifaa cha umeme tayari ni shilingi elfu 36,000/= ukijumlisha na vat elfu 27,000/= jumla yake ni shilingi 63,000/= na gharama ndogo ndogo za waya na fundi aliyesajiliwa basi umeme una waka kwako”. Alisema Bw. Chowo
Kwa upande wake Afisa Mkuu wa Afya Mahali pa Kazi Bw.. Fred Kayega alieleza suala zima la mfumo wa umeme kwa Wateja wote walio tembelea banda la TANESCO. “Mteja anatakiwa kufanya ukaguzi wa mfumo wa umeme kwenye nyumba yake, kila baada ya miaka mitano ilikujua kama mfumo mzima bado unafanya kazi wa ufanisi Zaidi”. Aliongeza.
Mbali na hayo, Bw. Kayega aliongelea suala zima la adhari za mashine umba(Tranfoma) na mafuta kutokana na maswali ya Wateja wengi waliotembelea banda la TANESCO, alitoa ufafanuzi kwa kusema mafuta ya tranfoma yana sifa kuu mbili moja  ukaaji wake ni muda mrefu na pili kazi ya mafuta hayo ni kupooza umeme unaoingia kutoka laini kubwa na kusambazwa kwa Wateja kutoka 33kv mpaka 11kv, lakini pia yanaadhari kwa Afya ya Binaadamu, Kwa upande mwingine alieleza pia aina ya tranfoma ambazo zinatumia joto na zinazotumia upepo kupooza umeme,na kusema kwasasa shirika limeanza kuingiza transfoma za joto za kupoozea umeme.
Aidha Mtaalamu wa Afya na Usalama Kazini, Ndugu Nelson Mnyanyi kutoka makao makuu, aliongelea kuhusu vifaa mbalimbali wanavyotumia ili kuhakikisha Usalama na Afya kwa wafanyakazi ndani ya Shirika ambavyo hutumika katika shughuli zao pindi wakiwapo katika maeneo yao ya kazia, aliongelea juu ya kifaa cha “Hand held x- ray spectrometer” kifaa ambacho hutumika kupima kiasi cha dawa iliyoingia katika nguzo kama kinakidhi au kutokukidhi kulingana na viwango “Spesifications” zilizowekwa na TANESCO, “Environmental Meter” Kifaa ambacho hutumika kupima kiwango cha kelele, joto, kiasi cha cha mwanga na kiasi cha maji yaliyopo angani “humidity’’. Kifaa kingine alichofafanua ni cha “alcohol tester” ambacho hutumika kupimia wafanyakazi kujua kama wamelewa au hapana na kwa kiwango gani mfanyakazi amelewa au hapana.
Kwaupande mwingine ,Mhandisi kutoka Idara ya Masoko Ally Koyya alifafanua juu ya matumizi bora ya nishati ya umeme majumbani kwakutumia vifaa ambavyo vinakidhi na kuleta usalama majumbani, mafunzo hayo ikiwemo aina mbali mbali za taa, jokofu, jiko la umeme,  pamoja na kufafanua uhai wa maisha ya kila kifaa na faida zake.
Hatahivyo wakazi wa Moshi mjini, walifurahishwa na Maelezo pamoja na  elimu inayotolewa, na kusema wamejifunza mengi waliyokuwa hawayafahamu kuhusu TANESCO nakuomba elimu iwekewe mkazo na jamii itapata uwelewa mkubwa kupitia wao.
Huku wakishinikiza maneno ya Mhe. Rais walioyasikia kuhusu neno “Ka-ta” na kusema kwa hali hii wanaunga mkono hoja na kwa maendeleo ya Taifa kuelekea uchumi wa viwanda.