March 2, 2018

NAMBA ZA MADAWATI YA DHARURA -TANESCO DAR ES SALAAM




ILALA-CITY CENTRE

0222133330/ 0784 7685860715 768586

WILAYA YA TABATA

0684 001068/ 0715 768589

WILAYA YA GONGO LA MBOTO

0688001071/ 0715768584 

WILAYA YA VIWANDA/TAZARA

0684001066/ 0715768587

WILAYA YA YOMBO

0783360411/0765654767

MKOA WA KINONDONI KUSINI/MAGOMENI

0784271461/ 0715271461

WILAYA YA KIMARA

0788379696/ 0717379696

MKOA WA KINONDONI KASIKAZINI/MIKOCHENI

0784 768584/ 0716 768584

WILAYA YA MBEZI BEACH

0658 768583/ 0713 768581

WILAYA YA TEGETA

0658 768584/ 0717 650 878

MKOA WA TEMEKE/KURASINI

0222138352/ 0732 997361/ 0758881055/ 0712 052720

WILAYA YA KIGAMBONI

0788499014/ 0736501661

WILAYA YA MBAGALA

0714 073 588

KITUO CHA MIITO YA SIMU/CALL CENTRE

0768 985 100/0222194400
  
MITANDAO YA KIJAMII

Facebook: Like
www.facebook.com/tanescoyetu

Twitter:Follow
www.twitter.com/tanescoyetu

Webiste
www.tanesco.co.tz

Barua pepe
Customer.service@tanesco.co.tz


"TANESCO TUNAYAANGAZA MAISHA YAKO"

March 1, 2018

Mhe. Mgalu awasihi Wananchi Mkoani Shinyanga kuupokea mradi wa Umeme Vijijini


Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Subira Mgalu,  amefanya ziara ya kikazi katika Vijiji Vitakavyopitiwa na Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III) na vile vilivyopendekezwa katika Mradi kabambe wa kuongeza wigo (REAII Densification) vilivyopo Mkoani Shinyanga.

Katika Ziara hiyo, Mhe. Mgalu  aliwasihi Wananchi kuupokea mradi huo na kuongeza kuwa Serikali itahakikisha Vijiji vyote vilivyobakia wilayani humo vitapata umeme kufikia 2020.

Aidha, Naibu Waziri alitumia ziara hiyo kukitambulisha kifaa cha Umeme Tayari  (UMETA) na kuwasihi Wananchi kujitokeza kwa wingi pindi mradi wa "Densification" utakapoanza  na kuitaka TANESCO kuhakikisha inashirikiana kwa karibu na Viongozi wa Serikali katika ngazi zote ili kuhakikisha miradi kwenye Vijiji vyote  unatekelezwa kwa weledi huku vipaumbele ikiwa ni Taasisi za Serikali na zile za Kidini.

 Kwa upande wake Meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga Mhandisi FedGrace Shuma alimhakikishia Naibu Waziri kuwa, atahakikisha miradi katika Vijiji vyote unakamilika kwa ufanisi kama ambavyo Serikali imeagiza, kwa kuzingatia huduma iliyoboreshwa.
 
Katika ziara hiyo Naibu Waziri aliambatana na Wakuu wa Wilaya za Kahama na Shinyanga, REA, TANESCO (Mkoa na Kanda) Viongozi wengine wa Serikali Mkoa na Wilaya pamoja na wadau kutoka Taasisi zingine Wilayani Kahama na Shinyanga.