April 24, 2012

HASARA KUBWA KWA TANESCO


  • Nguzo 22 zaanguka kwa upepo mkali
Shirika la Umeme Tanzania TANESCO limepatwa na tatizo la kuanguka kwa nguzo 22 za umeme eneo la Kipawa – Uwanja wa Ndege jijini  DSM kulikosababishwa na upepo mkali uliovuma kutoka eneo linalojengwa uwanja wa ndege wa Mwl. J.K.  Nyerere (Terminal III).

April 12, 2012

TUTAWAONDOA WALIOVAMIA NJIA ZA UMEME-MKUU WA MKOA DSM


Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Sadick. wa kwanza toka kushoto ni  Mkurugenzi Mtendeja Tanesco, Eng. William Mhando na Kulia ni Kamanda wa Kanda Maalum, Afande Kova.


Baada ya zoezi la kuwaondoa wafanyabiashara ndogo ndogo waliokuwa wamevamia maeneo yanayozunguka mitambo ya umeme na jengo la Makao Makuu ya TANESCO (Umeme Park), kufanikiwa Kamati ya ulinzi na usalama kupitia mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Said Sadik zoezi hilo ni endelevu kwa maeneo yote yaliyovamiwa.