December 24, 2017

HUDUMA ZETU KIPINDI CHA SIKUKUU









Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawatakia Wateja wake heri ya Sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya wa 2018.

Katika kusherehekea msimu huu wa Sikukuu, Shirika limejipanga kuhakikisha Wateja wetu mnaendelea kupata huduma bora na za uhakika saa 24.

Huduma zetu za dharura (Emergency) na Huduma kwa Wateja (Customer Care) zitapatikana muda wote.

Tunawaomba Wateja wetu kutupatia taarifa zitakazosaidia Wataalamu wetu kukufikia wa wakati kupitia kituo cha Miito ya Simu, Naba za Mikoa na Wilaya pamoja na mitaandao ya kijamii.

Imetolewa na: Ofisi ya Uhusiano
                        TANESCO Makao Makuu.

December 21, 2017

BODI YA WAKURUGENZI TANESCO YATEMBELEA MIKOA YA KUSINI


Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ikiongozwa na Mwenyekiti wake Dk. Alexander Kyaruzi (Pichani anayesaini) na baadhi ya Viongozi Waandamizi wa TANESCO, imefanya ziara katika Mikoa ya Kusini.

Lengo la ziara ziara hiyo ni kukagua sambamba na kujionea kasi ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme inayoendelea katika Mikoa hiyo ikiwemo miradi ya kufua umeme na ile ya usafirishaji.

Aidha, ziara hiyo imetumika kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali za Wateja wa Shirika.



December 15, 2017

Dkt. Kalemani aendelea na ziara ya kukagua maendeleo ya miradi ya umeme





Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani ameendelea na ziara ya kukagua hatua iliyofikiwa katika ukamilishaji wa ujenzi wa vituo vya kupoza na kusambaza umeme pamoja na njia ya kusafirisha umeme kutoka Makambako hadi Songea.

Lengo la ziara hiyo ni kukagua uimara wa mitambo ili Serikali kupitia TANESCO iweze kujipanga vizuri kwa kuwa na umeme wa uhakika.

"Kama ilivyo azma ya Serikali ya Awamu ya Tano kuifanya Tanzania kuwa nchi ya Viwanda, tunahitaji kuwa na umeme wa uhakika". Alisema Dkt. Kalemani.

Katika ziara hiyo pia amekagua miradi ya umeme Vijijini Awamu ya Tatu inayoendelea katika Mikoa hiyo ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati.

Akikagua mradi wa kusafirisha umeme wa msongo wa kilovolti 220 kutoka Makambako hadi Songea, Dkt. Kalemani alisema mradi huo utaiunganisha Mkoa wa Ruvuma katika Gridi ya Taifa.

Pia, kukamilika kwa miradi hiyo kutaipunguzia gharama Serikali kwa kuondokana na mitambo ya mafuta. 






December 14, 2017

Dkt. Kalemani " Serikali ya Awamu ya Tano imekusudia kuleta maendeleo kwa Wananchi"

Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani







 
Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani akiwa katika ziara ya kukagua mitambo ya kuzalisha umeme kwa njia ya gesi asilia Mkoani Mtwara, amekitembelea Kijiji cha Kalipembe kitakacho nufaika na mradi wa umeme Vijijini Awamu ya Tatu.

Kijiji hicho kipo Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara, ambapo Wananchi wamekuwa wakihitaji na adha ya kutokuwa na umeme licha ya njia ya imepita kuelekea Wilaya ya Newala miaka 18.

Dkt. Kalemani akiambatana na Viongozi wa TANESCO na REA aliwahakikisha Wananchi wa Kijiji hicho kupata umeme kupitia Awamu ya Tatu ya umeme Vijijini.

"Ndugu zangu Wananchi kazi yetu ni moja tu kuhakikisha mnapata umeme,  Serikali ya Awamu ya Tano imekusudia kuleta maendeleo kwa Wananchi wote, bila kujali itikadi kwani suala la maendeleo halina vyama". Alisema Dkt. Kalemani.

Aidha,  alitoa maagizo kwa Mkandarasi kuanza kazi mara moja ya kuchimbia nguzo, na kuutekeleza mradi huo bila kuruka Kijiji, Kitongoji hata Kaya, ambapo Mkandarasi aliahidi kuanza kazi mapema Wiki ijayo.

Akiongelea hali ya upatikanaji wa umeme Mikoa ya Lindi na Mtwara, Dkt. Kalemani alisema hivi sasa Mkoani wa Mtwara hakuna tatizo la umeme baada ya Matengenezo kukamilika.

"Kwa Mkoa wa Lindi tumeunda tume ya watu wa tano ili kufuatilia tatizo lipo sehemu gani katika miundobonu, tunawaahidi hali kuimarika baada ya muda mfupi". Alisema Dkt. Kalemani.

Aliongeza, Mikoa ya Kusini inatarajiwa kupata suluhisho la kudumu la tatizo la umeme itakapoingizwa katika Gridi ya Taifa, ambapo mwakani Mwezi Aprili inatarajiwa kituo cha Kuzalisha umeme cha Megawati 300 kuanza kujengwa.

Dkt. Kalemani anaendelea na ziara yake ambapo amekagua kituo cha kuzalisha umeme cha Tunduru, na cha Namtumbo vilivyopo Wilaya ya Ruvuma akiwa anaelekea katika Mradi wa Makambako - Songea.






December 10, 2017

TANESCO YAWATOA HOFU WATEJA WAKE JUU YA MFUMO WA UNUNUZI WA LUKU


Kaimu Meneja wa Teknolojia na Mawasiliano(TEHAMA)  wa Shirika la Umeme nchini Tanesco, Demetruce Dashina Akizungumza na Waandishi mara baada ya kuimarika kwa mfumo wa kununua Umeme kwa njia Luku
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limewatoa hofu Wateja wake juu ya mfumo wa ununuzi wa umeme kwa njia ya LUKU na kusema kuwa kwa sasa upo sawa na Wateja wanaweza wanaweza kufanya manunuzi katika njia za Maxcom, Mpesa, Halotel Money, Tigo Pesa, Selcom, Airtel Money, NMB na CRDB.

Akizungumza mapema leo jijini Dar es Salaam Kaimu Meneja wa Teknolojia na Mawasiliano (TEHAMA), Bw. Demetruce Dashina amesema kulitokea tatizo dogo la mfumo wa ununuzi wa umeme kwa njia ya LUKU wakati wa kuhamisha mfumo huo kutoka Ofisi ya zamani kwenda sehemu nyingine.

“Jana tulikuwa tunafanya uhamisho wa mfumo wa LUKU kwende katika Ofisi zetu mpya hivyo Wateja wetu walipata usumbufu kidogo, lakini kuanzia saa saba mfumo huo umekaa sawa na wateja wanaweza kununua umeme kama walivyokuwa wanafanya hapo awali bila shida yoyote mara baada ya marekebisho ya kiufundi” alisema Dashina.

Aliongeza TANESCO ilijipanga kuwahudumia wateja wake kama kawaida wakati wa kuhamisha mitambo hiyo lakini Wananchi wengi wakapata taharuki hivyo kufanya mfumo wa ziada kuzidiwa kutokana na watu kununua umeme kuliko kawaida.

Kwa upande wake Kaimu Meneja  Uhusiano wa Bi. Leila Muhaji amewaomba radhi Wananchi kwa usumbufu uliojitokeza na kuwasisitiza kuwa sasa wanaweza kununua katika mifumo iliyozoeleka.

Bi. Muhaji amesema kuwa TANESCO inatambua umuhimu wa umeme hivyo   kuwataka watanzania kuwa na Imani na shirika lao kwani lipo kwa ajili ya kuwahudumia  kama inavyohitajika.




   Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania Tanesco, Leila Muhaji akifafanua jambo wakati wa Mkutano wake na Waandishi wa Habari juu ya kuimarika kwa Mfumo wa Ununuzi wa luku mara baada ya kuhamia sehemu nyingine. 


Waandishi wa habari habari walifika katika mkutano huo wakifatilia kwa Makini. --

December 9, 2017

TAARIFA YA KUHAMISHA MIFUMO YA LUKU

Tunawataarifu Wateja wetu kuwa, kutokana na kazi ya ubomoaji wa jengo la Ofisi za TANESCO Makao Makuu, Ubungo linaloendelea, leo Desemba 09, 2017 kutakuwa na kazi ya kuhamisha Mifumo ya LUKU (Servers).

Kutokana na kazi hiyo Wateja wetu hawataweza kununua umeme kati ya saa 4 usiku hadi saa 7 usiku.
Ahsanteni kwa ushirikiano wenu.

Tutaendelea kutoa taarifa zaidi.

Toa taarifa kupitia namba za simu zifuatazo:
Kituo cha miito ya simu 2194400 na 0768 985100

Tovuti: www.tanesco.co.tz
 
Mitandao ya Kijamii
www.facebook/tanescoyetultd
twitter.com/tanescoyetu
 
Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu
Desemba 09, 2017

December 5, 2017

Menejimenti yafanya ziara Kinyerezi II


Menejimenti ya TANESCO imefanya ziara ya kutembelea Kituo cha kuzalisha umeme kwa njia ya gesi asilia cha Kinyerezi II Megawati 240, inayotumia Teknolojia ya "combined cycle power".

Teknolojia ya "combined cycle power "  inawezesha mitambo kuzalisha umeme kwa kutumia gesi na  mvuke.

Lengo la ziara hiyo ni kujiridhisha kukamilika kwa mashine namba moja kabla ya kuiingiza katika Gridi ya Taifa.

Inatarajiwa Desemba 07, mwaka huu kiasi cha Megawati 30 zinaingia katika Gridi ya Taifa.

Asilimia 15 ya gharama ya mradi zimefadhiliwa na Serikali ya Tanzania na asilimia  85 ni fedha kutoka kwa wafadhili.

Asilimia 95 ya wafanyakazi ni Watanzania.

Gharama za mradi ni kiasi cha Usd 344,059,746.00.

Ujenzi wa kituo hiki ulianza Machi 2016 na kinatarajiwa kukamilika Septemba 2018 ambapo Megawati zote 240 zitakuwa zimeingia katika Gridi ya Taifa.