February 10, 2020

TAARIFA KWA UMMA: TAHADHARI KWA WANANCHI WANAOISHI PEMBEZONI MWA MKONDO WA MAJI YATOKAYO KWENYE VYANZO VYA KUFUA UMEME KWA MAJI VYA MTERA NA KIDATU



MKURUGENZI MTENDAJI TANESCO, DKT. TITO MWINUKA


TAARIFA KWA UMMA:


FEBRUARI 10, 2020

      
TAHADHARI KWA WANANCHI WANAOISHI PEMBEZONI MWA MKONDO WA MAJI YATOKAYO KWENYE VYANZO VYA KUFUA UMEME KWA MAJI VYA MTERA NA KIDATU


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linatoa tahadhari kwa Wananchi wanaofanya shughuli za kibinadamu pembezoni mwa mkondo wa maji yatokayo katika mabwawa ya kufua umeme kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
Kufuatia taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini (TMA) kuwa mvua bado zinaendelea na zipo juu ya wastani, TANESCO inafanya tathmini iwapo siku za usoni maji yahamie upande wa pili kwa ajili ya usalama wa Mabwawa na Mitambo.
TANESCO inatoa tahadhari hii muhimu kwa Wananchi hususani wale wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali za kiuchumi kama vile Uvuvi, kulisha Mifugo, Kilimo na shughuli nyingine kwenye mkondo wa mto, vidimbwi au pembezoni mwa bwawa kuacha kufanya shughuli za kibinadamu, kijamii na kiuchumi kwa kipindi hiki ambacho mvua za Vuli zikiwa zinaendelea kunyesha.

Hali ya Ufuaji umeme katika mabwawa ya Mtera na Kidatu unaendelea vizuri kwa asilimia mia moja (100%) na kiwango cha maji kimeongezeka kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha kuanzia mita 691.22 juu ya usawa wa bahari kuanzia Desemba 01, 2019 hadi kufikia mita 698.40 juu ya usawa wa bahari Februari 10, 2020 katika bwawa la Mtera.
Shirika litaendelea kuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi wote waishio maeneo ya pembezoni mwa mkondo wa maji na mabwawa ya Mtera na Kidatu kwa  ushirikiano na Viongozi wa Wananchi wa maeneo hayo.

TANESCO itaendelea kutoa taarifa mara kwa mara kadri hali ya mvua itakavyokuwa inaendelea.




Imetolewa na:  Ofisi ya Uhusiano
                          TANESCO-Makao Makuu


                                

No comments:

Post a Comment