August 27, 2020

Kampeni ya "PETA" yatatua kero za umeme Mkoani Tanga.

 

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Tanga hivi karibuni limezindua Kampeni ya "PETA" lengo likiwa ni kutoa elimu ya huduma zote zitolewazo na TANESCO ikiwemo kutatua kero mbalimbali za umeme kwa wananchi.

Akizindua kampeni ya PETA Kaimu Meneja Mkoa wa Tanga Mhandisi Bakari Kalulu akiambatana na wakuu wa Idara za TANESCO Mkoa wa Tanga ili kupokea Kero za Wananchi na kuzitolea majibu yake.


Mhandisi, Kalulu alisema baadhi ya Wateja wa TANESCO wanatumia umeme kwa ajili ya kufukuza giza yaani kwa ajili ya Taa tu, PETA imekuja na majibu ya kuwahamasisha wateja waache fikra hizo na kufikiri namna nzuri ya kutumia umeme kukuza vipato vyao na Taifa kwa ujumla.

Akiielezea Kampeni hiyo, Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja Mkoa wa Tanga, Bw. Amon Bandiwe alisema PETA ni kifupi cha maneno P =Pata , E =Elimu ya matumizi Bora ya umeme, T =Toa kero yako, A = Acha kuhujumu miundombinu.

Aliongeza, kampeni ya PETA itasaidia TANESCO kufikia malengo ya utoaji wa huduma ya umeme kwa Wateja na ni chachu ya kubadili fikra za Wateja kwa kutumia nishati ya umeme kukuza vipato vyao.

Kampeni hii ni suluhisho la changamoto zote za kero zinazotokana na huduma ya umeme Mkoani Tanga.

Wakazi wa Mkoa wa Tanga wameipongeza TANESCO kwa kuzindua kampeni ya PETA kampeni ambayo itaisaidia TANESCO Mkoa wa Tanga kuboresha huduma zake kwa Mkoa na Wilaya.

Aidha, Jumla ya kero 21 zilipokelewa na kujibiwa na wakuu wa Idara papo kwa papo.





 


No comments:

Post a Comment