May 26, 2021

TANZANIA YAPATA DOLA MILIONI 140 UTEKELEZAJI MRADI WA UMEME MARAGARASI

 

Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Nishati na TANESCO, leo Mei 26,2021, imeingia makubaliano ya mkopo wa Dola milioni 140 kutoka Benki ya Maendeleo ya Africa (ADB) kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa kufua umeme wa megawati 49.5 kupitia maporomoko ya maji ya Mto Malagarasi uliopo Mkoani Kigoma.

Mradi wa Maragalasi utachochea ukuwaji wa shughuli za maendeleo ya kijamii pamoja na kiuchumi kwa wakazi wa Mikoa ya Kaskazini Mashariki mwa Tanzania.

Mradi huu, utahusisha pia uimarishaji gridi ya Taifa itakayorahisisha biashara ya mauziano ya Nishati ya umeme baina ya Tanzania na Nchi majirani.

Aidha gharama za mradi huo kwa ujumla ni takriban Dola milioni 144.14, ambapo Serikali ya Tanzania itachangia kiwango kinachobakia cha Dola milioni 4.14 kukamilisha fedha za Ujenzi wa Mradi huo muhimu kwa Mikoa ya ukanda wa Kaskazini Mashariki na Tanzania kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment