November 15, 2016

TANESCO YAAHIDI UMEME WA UHAKIKA KATIKA TANZANIA YA VIWANDA

Ziara ya hivi karibuni ya Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Felchesmi Mramba, alipotembelea kituo kipya cha kupoza na kusambaza umeme cha Ilala Mchikichini jijini Dar es Salaam

NA Henry Kilasila
KUONGEZEKA kwa shughuli za Kiuchumi pamoja na ongezeko la idadi ya Watu waliopatiwa Huduma ya umeme Nchini, kumefanya mahitaji ya umeme kuwa makubwa zaidi.

Mathalan takwimu zinaonesha, mahitaji ya juu ya umeme yameongezeka kutoka MW 988.27 Mwezi Desemba 2015 hadi kufikia MW 1,026.02 Mwezi Machi, 2016 sawa na ongezeko la asilimia 4.

Wizara ya Nishati na Madini kupitia Shirika la Umeme Nchini Tanzania (TANESCO), imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kuboresha Miundombinu ya umeme kote Nchini ili Wananchi waweze kupata umeme ulio bora na wa uhakika zaidi na hivyo kuemdana na malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano ambayo imedhamiria kujenga uchumi wa Viwanda.

Miongoni mwa hatua ambazo TANESCO imekuwa ikichukua ni pamoja na kukarabati na kubadilisha Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji umeme kwenye maeneo kadhaa ya Nchi.

Hali ya upatikanaji umeme Nchini kwa sasa imeendelea kuimarika siku hadi siku ukiachilia mbali katika baadhi ya maeneo Nchini ambayo umeme hukosekana kwa sababu ya hitilafu za muda mfupi pamoja na matengenezo yanayoendelea hivi sasa kote nchini ya kukarabati na kubadilisha Miundombinu ya umeme.
Kwa sasa uwezo wa mitambo ya kufua umeme (installed capacity) Nchini ni MW 1,439.97 ambapo MW 1357.69 ni mitambo iliyounganishwa katika Gridi ya Taifa na kiasi cha MW 82.28 ni mitambo iliyo nje ya Gridi (Isolated stations).Uwezo wa mitambo ya kufua umeme katika Gridi ya Taifa kwa kutumia nguvu za maji (hydropower)  ni MW 566.79 sawa na asilimia 41.70 ya mitambo yote. Mitambo itumiayo Gesi Asilia ni MW 607.00 sawa na asilimia 44.7 wakati Mitambo ya kufua umeme kwa kutumia mafuta ina uwezo wa MW 173.40  sawa na asilimia 12.8, na umeme unaofuliwa kwa kutumia biomass ni MW 10.5 sawa na asilimia 0.8 ya mitambo yote.
 
Katika kuhakikisha hali ya upatikanaji umeme Nchini itakayokwenda sambamba na malengo ya Serikali ya kujenga Uchumi wa Viwanda inaimarika zaidi, Wizara kupitia TANESCO imekuwa ikitekeleza sio tu Miradi ya Ufuaji umeme bali pia miradi ya njia za Usafirishaji na Usambazaji umeme.
Utekelezaji wa miradi hii uko katika hatua mbili za muda mfupi na muda mrefu ambapo baadhi ya Miradi tayari imekamilika na mingine iko katika hatua mbalimbali.

Miradi ambayo kwa asilimia kubwa tayari imekamilika ni pamoja na ile ya kuimarisha Miundombinu ya Kusambaza na Kusafirisha umeme katika Majiji na Miji hapa Nchini, ambayo ni;
Mradi wa kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Jiji la Dar es Salaam ambapo ujenzi wa kituo cha Kupoza umeme katikati ya Jiji upo katika hatua za mwisho za kukamimilika (Improving the Electricity Power Supply relability in City of Dar es Salaam), ambapo mradi huu unafadhaliwa na Serikali ya Finland pamoja na Serikali ya Tanzania.

Mradi mwingine ni ule wa Tanzania Energy Development and Access Project (TEDAP) unatekelezwa katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha na Kilimanjaro. Mradi unakusudia kuboresha na kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika katika mikoa husika . Mradi huu unahusisha ujenzi wa miundombinu ya kusambaza, kusafirisha pamoja na vituo vya kupoza umeme.
Mradi wa uzalishaji umeme uliokamilika ni ule wa ujenzi wa mitambo ya Kinyerezi I (MW 150) Mwezi Machi, 2016 na katika kipindi cha Mwaka 2016/17  ujenzi wa mitambo mipya ya Kinyerezi I Extension (MW 185) na Kinyerezi II (MW 240) umeanza kutekelezwa.
Utekelezaji wa ujenzi wa miradi hii ya uzalishaji umeme umekuwa ukienda sambamba na utekelezaji wa ujenzi wa miradi ya njia za kusafirisha na kusambaza umeme, kama ule wa kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Iringa hadi Shinyanga (backborne) ambapo upo katika hatua za mwisho kukamilika.
Mradi huu wa backborne utaimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo ya Kanda ya Ziwa, Kati na Kaskazini. Mradi huu umekamilika kwa asilimia 98 hadi hivi sasa.
Pia kuna Mradi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Makambako hadi Songea wa msongo wa kilovoti wa 220 wenye urefu wa kilomita 250 pamoja na kusambaza umeme katika mikoa ya Njombe na Ruvuma. Kazi zinazoendelea ni ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme.
kwa upande wa njia ya kusafirisha umeme, kazi zinazoendelea ni usanifu wa kina (Detail Feasibility Study), uingizwaji wa vifaa vya ujenzi na uandaaji wa eneo la mradi (Site Moblization).

Lakini pia TANESCO inatekeleza miradi mwingine wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 400 yenye urefu wa kilomita 1,148 kutoka Mbeya - Sumbawanga- Kigoma - Nyakanazi (North - West Transmission Line);

Kwa upande wa Kaskazini mwa nchi yetu TANESCO inatekeleza Mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 400  yenye urefu wa kilomita 664 kutoka Dar es Salaam - Chalinze – Tanga - Arusha (North - East Transmission Line). Kazi zinazoendelea kwa sasa ni kuweka mipaka kwenye njia ya kusafirisha umeme;

Mradi mwingine ni wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Somanga fungu hadi Dar es Salaam (Kinyerezi), gharama za mradi ni Dola za Marekani milioni 150. Kwa sasa Serikali inatafuta fedha za kutekeleza mradi husika;
Sekta binafsi nayo haikuachwa nyuma katika harakati za uzalishaji na usafirishaji umeme nchini.
Kwa kuzingatia kuwa azma ya Serikalini kufikia uzalishaji wa umeme wa Megawati 5,000 ifikapo 2020 na Megawati 10,000 ifikapo 2025. Serikali ilianzisha mkakati maalum wa kuongeza uwekezaji katika miradi ya kuzalisha umeme ambayo inatekelezwa kwa kushirikiana na sekta binafsi kutoka ndani na nje ya nchi.

Kwa upande wa miradi ya uzalishaji umeme, sekta binafsi imeshirikishwa katika miradi midogo ya Nishati Jadidifu (Renewable Energy) yenye MW 16.29 imetekelezwa na sekta binafsi, nayo ni Miradi midogo ya kuzalisha  umeme wa maji (Min Hydropower) ambayo ni Uwemba- MW 0.84; Mwenga MW 4; na Yori MW 0.95; na Miradi midogo ya kuzalisha umeme kwa kutumia tungamo taka (Biomass) ni Tanwat MW 1.5 na TPC MW 9.0.
 
Kilwa Energy Gas Fired Plant (371.2 MW)- US$ Milioni 465, Mwekezaji yupo katika hatua za mwisho za majadiliano ya Mikataba mbali mbali ambayo ni; Mkataba wa nyongeza wa utekelezaji (Addendum to Implementation Agreement), Mkataba wa Ubia (Shareholders Agreement), na Mkataba wa kununua gesi asilia (Direct Gas supply Agreement) ili kupata ufadhali wa mradi.
Kwa upande wa Miradi ya usafirishaji umeme, uwekezaji kwenye miundombinu ya usafirishaji wa umeme ni jukumu la Serikali na si sekta binafsi. Aidha, Sheria ya umeme ya Mwaka 2008 inaruhusu sekta binafsi kupitisha umeme kwenye miundombinu hiyo kwa kulipia Wheeling Charge na wala si kumiliki miundombinu husika.
Hatua hizi za Wizara ya Nishati na Madini kupitia TANESCO hazikuishia kuboresha upatikanaji umemem mijini tu bali pia vijijini, ambapo kupitia mpango wa kusambaza umeme vijijini REA ambapo sasa mpango huo uko katika awamu ya tatu (REAIII). Miradi mbalimbali inatekelezwa ikiwa ni pamoja na kukamilika kwa mradi wa Turnkey Phase II.

Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Pili umekamilika kwa asilimia 92.5%. Ambapo, wateja 110,868 kati ya 257, 000 wameunganishiwa umeme sawa na asilimia 43%;
Wilaya mpya 13 zimepatiwa umeme: Busega, Buhigwe, Chemba, Itilima, Kakonko, Kalambo, Kyerwa, Mkalama, Mlele, Momba, Nanyumbu, Nyasa na Uvinza;
Lakini pia Mradi kabambe wa kupeleka umeme Vijijini (REA Turnkey Phase III) unaotekelezwa katika kipindi cha miaka mitano (5) kuanzia 2016-2020, inategemewa vijiji vyote hapa nchini vitapata huduma ya umeme baada ya kukamilika kwa mradi huu.

Mpaka sasa upatikanaji wa Huduma ya umeme  (electricity access level) kitaifa umekua na kufikia asilimia 40, ambapo Wananchi  waliounganishwa na Huduma ya umeme (electricity connection level) ni asilimia 36 (Juni, 2016).

Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA TURNKEY PHASE III).
Mradi huu utatekelezwa kwa kipindi cha miaka 5 katika vijiji 7,873 vya wilaya zote za Tanzania Bara. Takribani Vijiji 7,697 vitapelekewa umeme wa Gridi ya Taifa na Vijiji 176 umeme wa nje ya Gridi (Off-grid).
Mpango huu utaongeza wigo wa Usambazaji umeme katika maeneo ambayo hayakufikiwa na Mradi wa REA Turnkey Phase II. Wakandarasi watakaojenga Miundombinu ya Mradi huu wameshapatikana. Shilingi Bilioni 587.61 zimetengwa kutekeleza Mradi huu katika kipindi cha Mwaka 2016/17. Kati ya fedha hizo Shilingi bilioni 534.40 ni fedha za ndani na Shilingi Bilioni 53.21 ni fedha za nje.
Serikali kupitia TANESCO pia inaendelea kuhimiza Wananchi kuunganisha Huduma ya umeme katika maeneo yao ya Vijijini hii ni baada ya utekelezaji wa Miradi Kabambe ya REA kufanikiwa kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na kasi ya Wananchi ya kuunganisha Huduma ya umeme.






November 9, 2016

TANESCO YATOA TAARIFA KUFAFANUA KUHUSU BEI YA UMEME

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), Mhandisi Felchesmi Mramba

November 8, 2016

TAARIFA KWA UMMA



Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kutoa ufafanuzi kuhusu taarifa iliyotolewa katika vyombo mbalimbali vya habari kuhusu ombi la kurekebisha bei za umeme kwa mwaka 2017.
 
Ombi la mabadiliko ya bei za umeme liliwasilishwa EWURA kulingana na Agizo la kubadilisha bei za umeme la mwaka 2016 lililoanza kutumika tarehe 1 April 2016. Ifahamike kuwa bei za umeme (Electricity Tariffs) zinazotumika zilitolewa zitumike mpaka tarehe 31/12/2016, hivyo itakapofika Januari 2017, inatakiwa bei mpya za umeme (New Electricity tariff) kutolewa kwa mujibu wa sheria. 

Hivyo TANESCO ilitakiwa kufanya tathmini ya gharama  za uzalishaji , usafirishaji na usambazaji umeme na kupeleka mapendekezo hayo kwenye Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji(EWURA), ili kupitiwa na kufanyiwa taftishi(kupata maoni ya wadau) ikiwa ni pamoja na Baraza la Ushauri la Serikali . Hivyo basi ikiwa bei za umeme    zitapanda au kutopanda, hiyo itategemea na mapitio ya tathmini ya gharama za kuzalisha, kusafirisha na kusambaza umeme tulizo wasilisha EWURA.

TANESCO haiwezi kuamua yenyewe kupandisha au kutopandisha bei za umeme. Kwa mujibu wa sheria, EWURA inapaswa ifanye mapitio ya bei za umeme kwa kila robo mwaka (Periodic Tariff Adjustment).

Tunapenda Umma ufahamu kuwa kupanda au kushuka kwa gharama za umeme ni suala la kisheria na ni jambo la kawaida kwani bei ya umeme imeshawahi kushuka katika vipindi tofauti kwa mfano Mwaka 2015 (robo ya kwanza ya mwaka) bei ilishuka kwa asilimia 2.5.  Vivyo hivyo Mwezi Aprili mwaka 2016 pia gharama za umeme zilishuka kwa asilimia 1.6


IMETOLEWA NA:  Mhandisi FELCHESMI MRAMBA
                                    Mkurugenzi Mtendaji
                                     Shirika La Umeme Tanzania (TANESCO)
                                     08 Novemba 2016

MKURUGENZI MTENDAJI WA TANESCO, MHANDISI FELCHESMI MRAMBA, ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA KINYEREZI II

MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Felchesmi Mramba, (mbele kulia), akikagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa gesi wa Kinyerezi II jijini Dar es Salaam


MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Felchesmi Mramba, (anayezungumza pichani), amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa mradi wa umeme wa gesi wa Kinyerezi II utakaozalisha umeme wa Megawati 240 unaotekelezwa na shirika hilo jijini Dares Salaam.
Mradi huo ulizinduliwa Machi 2016 kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. John Pombe Magufuli, kuweka jiwe la msingi  ambapo eneo hilo lilikuwa pori tu kazi ya kusafisha eneo ili kuanza ujenzi ilianza mieziminane iliyopita.
“Kwa wale waliokuwepo siku Mheshimiwa Rais anaweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi huu, mtakumbuka kuwa eneo lote hili lilikuwa pori, napenda niwapongeze wahandisina mafundiwote mnaotekeleza ujenzi huu kwa kazi nzuri nakasi ya kuridhisha.” Alipongeza Mhandisi Mramba, ambaye alitembelea eneo hilo mwishoni mwa wiki kukagua maendeleoyaujenzi wake.
Wahandisi wa TANESCO wakishirikiana na wenzao kutoka SUMITOMO CORPORATION NA TOSHIBA za Japan na washauri wa mradi Lahmeyer International ya Humburg nchini Ujerumani, ndio wanaojenga mitambo hiyo kwa ambapo unatekelezwa kwa fedha za walipa kodi wa Tanzania na Japan.
Akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi huo, Meneja Mradi, Mhandisi Stephen Manda alisema ni pamoja na ujenzi wa msingi wa kitalu namba moja (Foundation Works Block I na ujenzi wa msingi watenki la kuhifadhia maji (raw water tank).
“Kazi inaendelea vizuri napenda kukujulisha kuwa baadhi ya vifaa muhimu vimekwisha wasili na tunachosubiri pengine kufikia mwezi Januari ni kuwasili kwa mashine zenyewe (Turbines), hivi sasa tuko kwenye mazungumzo na watu wa TANROAD na mamlaka nyingine kuhusu utaratibu wa kusafirisha mitambo hiyo kutoka bandarini kuiletahapa.” Alifafanua Mhandisi Manda.
Akielezea zaidi kuhusu manufaa ya mradi huo pindi utakapokamilika, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhanidis Felchesmi Mramba alisema, TANESCO iliwaahidi watanzania kuwa kwa kushirikiana na serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya umeme ikiwa ni pamoja na kuzalisha umeme mwingi zaidi ili hatimaye uende sambamba na malengo ya serikali yaawamu ya Tano ambayo imedhamiria kujenga nchi ya viwanda.
“Nia yan Mheshimiwa rais ya kujenga nchi ya viwanda itafanikiwa kwa vile sasa umeme mwingi na wa uhakika utapatikana ili kuhudumia viwanda vilivyopo na vipyavinavyoendelea kujengwa.”Alihitimisha Mhandisi Mramba.


 Mhandisi Mramba, (kulia), akiongozana na Meneja Mradi wa ujenzi wa Kinyerezi II, Mhandisi Stephen Manda
 Ujenzi wa msingi wa tenki la kuhifadhia maji (raw water tank)
 Ujenziwa msingi wa moja ya sakafu ya kufunga mashine za kufua umeme, (Foundation work block)

 Mhandisi Manda, (kulia), akifafanua masuala mbalimbali yahusuyo maendeleo ya ujenzi huo
 Mhandisi Manda akiwasilisha taarifa ya hatua mbalimbali za ujenzi wa mradi huo
 Jengo la muda la utawala
 Kazi ya kuhamisha kifusi ikiendelea
 Mhandisi Manda aakionyesha kitu
 Meneja Mwandamizi wa TANESCO anayeshughulikia miradi ya usafirishaji na usambazaji umeme, Mhandisi Gregory Chegere (kulia), akizungumza jambo na mmoja wa Wahandisi viongozi kutoka kampuni ya TOSHIBA ya Japan
 "Mambo swafi" ndivyo anavyoonekana akisema, Mhandisi Mramba, wakati akianza ukaguzi wa mradi huo akifuatana na Meenja Mradi, Mhandisi Manda (kushoto)
 Mameneja na maafisa wa TANESCO waliofuatana na Mkurugenzi Mtendaji kutembelea eneo hilo
 Mhandisi kiongozi wa kampuni ya TOSHIBA
Mameneja na maafisa wa TANESCO

November 7, 2016

Quotation No: PA/001/2016-17/HQ/N/32



Repair and Service of GPRS, Gas Boiler and Instruments Including Controls/ Sensors at Kinyerezi I Gas Plant under Framework Contract

INVITATION FOR QUOTATIONS

                                                                                                                 Date: November, 2016


  1. This Invitation for Quotations (IFQ) follows the General Procurement Notice for this project which appeared in the Daily News Paper dated 3rd August, 2016.

  1. The Tanzania Electric Supply Company Limited (TANESCO) has set aside funds for its operations during financial year 2016 / 2017 and it intends to apply part of the proceeds of this funds to cover eligible payments under the contract for which this invitation is issued.

  1. TANESCO now invites sealed quotations from eligible bidders for Repair and Service of GPRS, Gas Boiler and Instruments Including Controls/ Sensors at Kinyerezi I Gas Plant under Framework Contract. 
  1. The Invitation for Quotation will be conducted through the Competitive Quotation procedures specified in the Public Procurement Regulations, 2013 – Government Notice No. 446. 
  1. Interested eligible Bidders may obtain further information and/or inspect the Quotation Document at the office of the Procurement Management Unit located at Ground Floor, Room No. G15, TANESCO Head office, Umeme Park Building, Ubungo, along Morogoro Road, P.O. Box 9024 Dar es Salaam. Telephone + (255) 0782 376147 from 09:00hrs to 16.00hrs on Mondays to Fridays inclusive with an exception of public holidays.
  1. A complete set of Quotation Document in English and additional sets may be purchased by interested Bidders on the submission of a written application to the address given under paragraph 5 above and upon payment of a non-refundable fee of TZS 50,000.  
7.      All quotations must be accompanied by a Tender Securing Declaration in the format provided in the Quotation Document.
8.      Performance Security of 10% of contract price in the Form of Bank Guarantee shall be submitted within fourteen (14) days of receipt of the notification of contract award.
9.      All quotations in one original plus three copies, properly filled in, and enclosed in plain envelopes clearly markedADVERTISMENT OF QUOTATION No. PA/001/2016-17/HQ/N/32 FOR REPAIR AND SERVICE OF GPRS, GAS BOILER AND INSTRUMENTS INCLUDING CONTROLS/ SENSORS AT KINYEREZI I GAS PLANT UNDER FRAMEWORK CONTRACT(NOT TO BE OPENED BEFORE 10:30 HOURS on FRIDAY, 25TH NOVEMBER, 2016) should be addressed to the SECRETARY, TANESCO TENDER BOARD, P.O. BOX 9024, DAR ES SALAAM to reach him at Room No. G 15 not later than 10:30 HOURS local time on Friday, 25th November, 2016. Quotations will be opened thereafter in Public and in the presence of Bidders’ representatives who choose to attend in the opening at Twiga Board Room located at Ground Floor, TANESCO Head Offices, Umeme Park Building, Morogoro Road – Ubungo.
10.  Late quotations, Portion of quotations, Electronic quotations, Quotations not received, quotations not opened and not read out in Public at the tender opening ceremony shall not be accepted for evaluation irrespective of the circumstances.

MANAGING DIRECTOR
TANZANIA ELECTRIC SUPPLY COMPANY LIMITED