March 31, 2015

KUKANUSHA TAARIFA KUHUSU HUDUMA YA LUKU

SHIRIKA LA UMEME TANZANIA- TANESCO

KUKANUSHA TAARIFA KWAMBA HUDUMA YA LUKU ITAKOSEKANA KWA WIKI MBILI

Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) linakanusha taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya jamii kwamba huduma ya kununua umeme kwa LUKU itasitishwa kwa wiki mbili.Taarifa hizi ni za uongo na zinazolenga kuharibu taswira ya shirika katika jamii.Mifumo yote ya LUKU ipo salama kabisa na Tanesco tunaendelea kuwahudumia wateja wetu kama kawaida.

Tunawaomba wateja wetu kuzipuuza taarifa hizo.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu.

No comments:

Post a Comment