March 26, 2019

Matengenezo kituo cha Ubungo II yameendelea

Machi 26, 2019



Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake wa Mkoa wa Dar es salaam na Zanzibar kuwa matengenezo kinga ya mashine namba 3 ya Kituo cha Ubungo II yanaendelea

Aidha, Kampuni ya Songas imeanza matengenezo makubwa yanayoenda sambamba na kubadilisha "engine" ya mashine namba 3 baada ya muda wake kuisha kuanzia tarehe Machi 25, 2019 na yanayotarajiwa kukamilika Aprili 09, 2019.

Kutokana na matengenezo hayo  baadhi ya maeneo ya Mikoa ya TANESCO ya Dar es Salaam ambayo ni Kinondoni Kaskazini, Kinondoni Kusini, Temeke na Ilala pamoja na Zanzibar yatakuwa na upungufu wa umeme na hivyo kuathiri maeneo hayo kwa nyakati tofauti.

TANESCO itaendelea kutoa taarifa ya Maendeleo ya kazi ya matengenezo ya kituo cha Ubungo yenye lengo la kuwezesha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa Dar es Salaam na Zanzibar kwa siku zijazo.

Kituo cha miito ya simu 2194400 na 0768 985100

Tovuti: www.tanesco.co.tz,

*Mitandao ya kijamii*

Twitter, www.twitter.com/tanescoyetu,

 Facebook https://www.facebook.com/tanescoyetultd/

*IMETOLEWA NA:*

OFISI YA UHUSIANO

TANESCO MAKAO MAKUU

No comments:

Post a Comment