May 2, 2019

Nyembo Mfanyakazi Bora TANESCO


Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wafanyakazi wakati wa Maadhimisho sherehe za Siku ya Wafanyakazi Duniani yanayofanyika Mkoani Mbeya Kitaifa, ambapo amewatoa hofu wafanyakazi na kuwahidi kuendelea kuboresha maslahi ya wafanyakazi kulingana na uwezo wa Serikali

Meneja  Kodi na Uzingatiaji Kanuni (Tax and Compliance Manager) TANESCO Makao Makuu Bw. Sepetu Nyembo, amechaguliwa kuwa Mfanyakazi Bora TANESCO kwa mwaka 2019 ambapo amepata zawadi ya fedha na cheti. 

Bw. Nyembo ametangazwa kuwa mfanyakazi bora katika maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) ambayo yamefanyika kitaifa kwenye uwanja wa kumbukumbu wa Sokoine jijini Mbeya na kuwa miongoni mwa wafanyakazi hodari waliopongezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwakabidhi vyeti.

Sherehe za mwaka huu kitaifa zimefanyika jijini humo ambapo inakadiriwa kiasi cha Wafanyakazi 6000 walishiriki kwenye sherehe hizo.

 Wafanyakazi walipita kwa  maandamano mbele ya Mheshimiwa Rais, Makamu wa Rais, mama Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa na viongozi wengine wa juu wa Serikali. 

Aidha, Mheshimiwa Rais na viongozi hao wa juu wa Serikali walipata fursa ya kuona misafara ya magari ya Taasisi mbalimbali za Umma na Binafsi yakionesha shughuli mbalimbali wanazofanya.
Sherehe za Mei Mosi, hutumika kama siku ya kukumbushana, kutafakari, kutathmini lakini pia kuzingatia wajibu kati ya wafanyakazi, waajiri na serikali ili kuleta matokeo chanya katika ujenzi wa taifa.


Bw. Sepetu Nyembo, ambaye ni Meneja Kodi na Uzingatiaji Kanuni(wapili kulia), akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wenzake kwenye ofisi za TANESCO jijini Mbeya ikiwa ni saa chache baada ya kutangazwa mfanyakazi bora wa mwaka wa TANESCO.








No comments:

Post a Comment