December 4, 2014

TAARIFA KWA UMMA




TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKOSEKANA KWA UMEME
KWA BAADHI YA MAENEO NCHINI

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linanapenda kutoa ufafanuzi kwa wateja wake kuhusu sababu za kukosekana kwa umeme kwa baadhi ya maeneo nchini kwa nyakati tofauti kama ifuatavyo:-

Mosi, Kuanzia Novemba 26, 2014 hadi Desemba 1, 2014 Mikoa yote iliyoungwa kwenye gridi ya taifa ilikuwa na upungufu wa umeme kwa baadhi ya maeneo kutokana na kuharibika kwa mashine moja ya Mtambo wa Kufua Umeme wa Kidatu yenye uwezo wa kufua megawati 50. Mtambo huo kwa sasa umetengamaa na hakuna Mkoa wenye upungufu wa umeme.

Pili, Novemba 29, 2014 Kulitokea hitilafu ya kulipuka na kuungua kwa Kikata Umeme (Circuit Breaker) kwenye Kituo cha Kupooza na Kusambaza Umeme cha Ubungo upande wa msongo wa kilovolti 33 na hivyo kusababisha gridi nzima ya taifa kutoka saa 11.38jioni na kurejesha saa 3.03 usiku kwa mikoa yote baada ya kutengeneza kifaa kilichoharibika. Hata hivyo baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Kinondoni Kusini (Magomeni) yaliendelea kukosa umeme kwa siku 2 mfululizo hadi tulipo funga Kikata Umeme kingine. Tatizo hilo limesha patiwa ufumbuzi na Mkoa huo kwa sasa unapata umeme kama kawaida.

Tatu, Kuanguka kwa nguzo kwa baadhi ya maeneo katika jiji la Dar es Salaam kutokana na kuanza kwa kipindi cha mvua.

Nne, Matengenezo yanayoendelea ya ukarabati wa miundombinu kwa mikoa yote ya nchini. Kazi zinazofanyika kwenye zoezi hilo kwa sasa ni kubadilisha nguzo zilizooza, kunyanyua nguzo zilizoinama, kuvuta nyaya zilizolegea na kukata miti inayogusa nyaya za umeme. Zoezi kama hili hufanyika kwa kila mkoa kwa nchi nzima kama tahadhari kabla ya kuanza kwa kipindi cha masika ambacho kinaambatana na mvua na upepo mkali.

Kwa sababu hii kubwa, kumekuwa na usumbufu wa kukatwa kwa umeme kwa baadhi ya maeneo kwa nyakati tofauti kulingana na ratiba ya mkoa husika ili kupisha zoezi hilo ambalo tunatarajia litakamilika mwezi huu wa Desemba.

Uongozi wa Shirika unaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza.

Imetolewa na
Ofisi ya Uhusiano,

December 3, 2014

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKOSEKANA KWA UMEME KWA BAADHI YA MAENEO KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM



Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linanapenda kutoa ufafanuzi kwa wateja wake kuhusu kukosekana kwa umeme kwa baadhi ya maeneo ya jiji la Dar es Salaam kwa sababu mbalimbali kama ifuatavyo:-

Mosi, Kuanzia Novemba 26, 2014 hadi Desemba 1, 2014 Mikoa yote iliyoungwa kwenye gridi ya taifa ikiwemo Dar es Salaam ilikuwa na upungufu wa umeme kwa baadhi ya maeneo kutokana na kuharibika kwa mashine moja ya Mtambo wa Kufua Umeme wa Kidatu yenye uwezo wa kufua megawati 50. Mtambo huo kwa sasa umetengamaa na hakuna Mkoa wenye upungufu wa umeme.

Pili, Novemba 29, 2014 Kulitokea hitilafu ya kuungua kwa Kikata Umeme (Circuit Breaker) kwenye Kituo cha Kupooza na Kusambaza Umeme cha Ubungo upande wa msongo wa kilovolti 33 na hivyo kusababisha baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Kinondoni Kusini (Magomeni) kukosa umeme kwa siku 2 mfululizo. Tatizo hilo limeshapatiwa ufumbuzi na Mkoa huo kwa sasa unapata umeme kama kawaida.

Tatu, Kuanguka kwa nguzo kwa baadhi ya maeneo katika jiji la Dar es Salaam kutokana na kuanza kwa kipindi cha mvua.

Nne, Matengenezo yanayoendelea ya ukarabati wa miundombinu kwa mikoa yote ya Dar es Salaam. TANESCO inaendesha zoezi la ukarabati wa miundombinu yake kwa mikoa ya Kinondoni Kusini (Magomeni), Kinondoni Kaskazini (Mikocheni), Ilala na Temeke. Kazi zinazofanyika kwenye zoezi hilo kwa sasa ni kubadilisha nguzo zilizooza, kunyanyua nguzo zilizoinama, kuvuta nyaya zilizolegea na kukata miti inayogusa nyaya za umeme. Zoezi kama hili hufanyika kwa kila mkoa kwa nchi nzima kama tahadhari kabla ya kuanza kwa kipindi cha masika ambacho kinaambatana na mvua na upepo mkali.

Kwa sababu hii kubwa, kumekuwa na usumbufu wa kukatwa kwa umeme kwa baadhi ya maeneo mara moja kwa siku ili kupisha zoezi hilo ambalo tunatarajia litakamilika mwezi huu wa Desemba.

Uongozi wa Shirika unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Imetolewa na
Ofisi ya Uhusiano,
TANESCO MAKAO MAKUU.

EMPLOYMENT OPPORTUNITIES INTERNAL & EXTERNAL ADVERTISEMENT



Background – TANESCO             http://www.tanesco.co.tz

Tanzania Electric Supply Company (TANESCO) is focusing on increasing the outreach and service quality of its Energy products for Tanzanians.  Next to its current passion as a leading provider of electricity is to be more efficient, customer focused utility for Tanzania and beyond. The Company has the largest electricity generation, transmission and distribution network in Tanzania. In order to reach its goals, the Company is investing heavily in its generation, transmission and distribution network, its business systems and human capital. TANESCO now invites applicants who are self-motivated, honest, hardworking and committed individuals to fill the under-mentioned posts.


Specific attributes for the Positions to be filled:
                          
All Candidates must:

v  Self motivated
v  Excellent communication skills
v  Creative, innovative and team working skills
v  High level of interpersonal skills
v  Demonstrate highest degree of integrity
v  Computer literacy will be an added advantage
                        
LIGHT CURRENT TECHNICIAN (1 POST)
     Reports To:  Electrical Engineer
     Reporting Office:  Mtera Hydro Power Plant


POSITION OBJECTIVE:

Execution of all planed maintenance works of Telecommunication systems in plants, grid, distribution substations and offices, with objective of ensuring smooth operational communication within the Plant.      

PRINCIPAL ACCOUNTABILITIES:

·         Inspect, test electronic and communication systems to ascertain their condition and operation status.
·         Prepare cost estimates and works orders for planned maintenance works of communication systems equipment.
·         Execute properly preventive maintenance works in a planned time to ensure emergence break downs are avoided.
·         Respond promptly to emergence calls during emergence break downs to ensure communication is restored within minimum time possible.
·         Install and perform proper commissioning of new installations as per required standards   to ensure proper systems operations.
·         Keep maintenance records, equipment status updating and observe reporting system to ensure a good data base and communication system.
·         Observe safety regulations and working procedures to ensure accidents to people and equipment are avoided.

ACADEMIC QUALIFICATION AND EXPERIENCE

  • Form IV or Form VI Secondary certificates
  • Ordinary Diploma or FTC in Electronics engineering from recognized institution
  • Minimum of 2-3 years’ experience post qualification with exposure to Power System
                       
Remuneration and Benefits:

Competitive remuneration package shall be offered commensurate with skills and experience. Details will be discussed at the interview; only people who fit the above criteria need to apply.

HOW TO APPLY:       
If you a Tanzanian National and interested in the position, you should send a written application giving full details of previous work life history, qualifications and include two work references. Applications should be marked “Private and confidential” and addressed to:

                                Plant Manager,
                                Mtera Hydro Plant,
                                P. O. Box 1
                                Mtera, Dodoma.
                                 Email: pm.mtera@tanesco.co.tz

   Application close date: Two weeks from the first appearance