November 14, 2017

TANESCO Makao Makuu yaikabidhi mchango wa Milioni Kumi Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete.



Leo  Novemba 14, 2017 Wafanyakazi wa TANESCO Makao Makuu wakiongozwa na  Meneja Mwandamizi kanda ya Dar es Salaam na Pwani Mhandisi Mahende Mugaya kwa Niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Dkt. Tito Mwinuka wamekabidhi hundi ya Shilingi Milioni kumi Taslimu kama mchango wa kugharamia matibabu ya watoto 5 wenye matatizo ya moyo katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete.

Mbali ya mchango huo wa Shirika wafanyakazi walichangia vifaa mbali mbali vya watoto kujikimu kama sabuni, maji ya kunywa, pampers n.k

Msaada huo ulikabidhiwa kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Profesa Mohammed Janab


No comments:

Post a Comment