August 11, 2021

MANUFAA YA KITUO CHA UMEME DEGE KWA KIGAMBONI NA MAENEO YA JIRANI


 Kituo cha kupokea na kupoza umeme  cha Dege ni mkombozi katika kukuza shughuli za kiuchumi na kijamii kwa Wilaya ya Kigamboni na maeneo jirani kutokana na kuimarisha upatikanaji wa umeme baada ya  kukamilika kwa utekelezaji wake Aprili 30, 2021.

Maeneo ya Viwandani, Pemba Mnazi, Mwasonga, Mwongozo, Kimbiji na maeneo jirani awali yalikuwa yanapata changamoto ya umeme kukatika au kuwa mdogo kutokana na njia ya umeme kusafiri umbali mrefu kutokea Mkoa wa kitanesco wa Ilala.

Akitembelea kituo hicho Agosti 07, 2021 Naibu Katibu Mkuu Nishati, Bw. Kheri Mahimbali ameridhishwa na usimamizi wa kituo cha Dege ambacho kilianza kujengwa Mei 02, 2019.

Aidha, mahitaji ya sasa ya Wilaya ya Kigamboni ni megawati 18 huku uwezo wa kituo cha Dege ni megawati 48 lakini malengo ya Serikali ni kukiongezea uwezo hadi hadi kufikia megawati 96.

 




 

No comments:

Post a Comment