August 11, 2021

NAIBU KATIBU MKUU AKAGUA MRADI YA UMEME LUGURUNI

 


Naibu Katibu Mkuu Nishati, Bw. Kheri Mahimbali, Agosti 07, 2021 alikagua utekelezaji wa mradi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Luguruni Jijini Dar es Salaam.

Utekelezaji wa mradi wa Luguruni ulianza Aprili 01, 2020 na unatarajiwa kukamilika Septemba 30, 2021 ikiwa ni miezi 18 ya utekelezaji wa mradi.

Kukamilika kwa mradi wa Luguruni kutaboresha hali ya upatikanaji wa umeme katika Mikoa wa Pwani na Dar es salaam hasa kwa maeneo ya Kimara, Mbezi, Hospitali ya Taifa ya Mloganzila, msigani, kibamba, kibwegere, kisarawe, Maili moja na TAMCO (Industrial area) ambayo yamekuwa na changamoto ya kukosekana kwa umeme wa uhakika kutokana na njia za umeme zinanipeleka maeneo hayo kusafiri umbali mrefu.

Gharama za uzalishaji mradi wa Luguruni ni Shilingi Bilioni 15.2 ambazo zinagharamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 





No comments:

Post a Comment