August 14, 2021

WAZIRI MKUU AKAGUA KITUO CHA TANESCO MSAMVU BAADA YA KUATHIRIKA NA MOTO

 

Waziri Mkuu wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, leo Agosti 14, 2021 amekagua kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Msamvu mkoani Morogoro.

Mhe. Majaliwa amekagua athari zilizotokea baada ya kupata hitilafu iliyopelekea kuwaka moto kwa jumba la kudhibiti mifumo ya umeme wa msongo wa kilovolti 33 Agost 2, 2021.

Aidha, amewataka Wafanyakazi wa TANESCO kuendelea kufanya kazi kwa uaminifu na weledi kutokana na nishati ya umeme kuwa ndio injini ya ukuaji uchumi wa Nchi.

" Watumishi wa TANESCO mmebeba mioyo ya watu, muongeze umakini katika utendaji wenu wa kazi", amesema Mhe. Majaliwa.

Katika hatua nyingine Mhe. Majaliwa ameiagiza TANESCO Kufanya mapitio ya Wafanyakazi wanaosimamia vituo vya kupokea na kupoza umeme ili kuhakikisha wanafanya kazi kwa weledi.

Kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Msamvu mkoani Morogoro ni moja kati ya vituo 51 ambavyo vinapokea na kupoza umeme mkubwa wa gridi ya Taifa.

 





 

No comments:

Post a Comment