September 4, 2021

MIRADI YA KIMKAKATI YA NISHATI ITAKAMILIKA KWA WAKATI

 

Naibu Katibu Mkuu Nishati, Bw. Kheri Mahimbali amesema miradi yote ya kimkakati ya umeme inayotekelezwa na Serikali kupitia TANESCO itakamilika kwa wakati.

Bw. Mahimbali ameyasema hayo leo Septemba 03, 2021 katika ziara ya Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri, kukagua vituo vya kuzalisha umeme kwa gesi vya Kinyerezi.

Amesema ziara ilijikita zaidi kwenye mradi wa Julius Nyerere, ambapo Sekretarieti iliweza kufahamu hatua zote za kuzalisha umeme hadi kuusafilisha.

"Leo tumewaonesha Kinyerezi complex ambayo ina Kinyerezi I, Kinyerezi I Extension pamoja na Kinyerezi ll" amesema Bw. Mahimbila.

Ametoa pongezi kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa inayoifanya katika kuendeleza miradi ya umeme nchini.

Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri inahitimisha leo ziara ya siku tatu kukagua miradi ya umeme, ziara ilianzia kwenye kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Zuzu Jijini Dodoma, njia ya umeme itakayojengwa hadi Chalinze na mradi wa kufua umeme kwa maji wa Julius Nyerere.





 

No comments:

Post a Comment