December 10, 2017

TANESCO YAWATOA HOFU WATEJA WAKE JUU YA MFUMO WA UNUNUZI WA LUKU


Kaimu Meneja wa Teknolojia na Mawasiliano(TEHAMA)  wa Shirika la Umeme nchini Tanesco, Demetruce Dashina Akizungumza na Waandishi mara baada ya kuimarika kwa mfumo wa kununua Umeme kwa njia Luku
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limewatoa hofu Wateja wake juu ya mfumo wa ununuzi wa umeme kwa njia ya LUKU na kusema kuwa kwa sasa upo sawa na Wateja wanaweza wanaweza kufanya manunuzi katika njia za Maxcom, Mpesa, Halotel Money, Tigo Pesa, Selcom, Airtel Money, NMB na CRDB.

Akizungumza mapema leo jijini Dar es Salaam Kaimu Meneja wa Teknolojia na Mawasiliano (TEHAMA), Bw. Demetruce Dashina amesema kulitokea tatizo dogo la mfumo wa ununuzi wa umeme kwa njia ya LUKU wakati wa kuhamisha mfumo huo kutoka Ofisi ya zamani kwenda sehemu nyingine.

“Jana tulikuwa tunafanya uhamisho wa mfumo wa LUKU kwende katika Ofisi zetu mpya hivyo Wateja wetu walipata usumbufu kidogo, lakini kuanzia saa saba mfumo huo umekaa sawa na wateja wanaweza kununua umeme kama walivyokuwa wanafanya hapo awali bila shida yoyote mara baada ya marekebisho ya kiufundi” alisema Dashina.

Aliongeza TANESCO ilijipanga kuwahudumia wateja wake kama kawaida wakati wa kuhamisha mitambo hiyo lakini Wananchi wengi wakapata taharuki hivyo kufanya mfumo wa ziada kuzidiwa kutokana na watu kununua umeme kuliko kawaida.

Kwa upande wake Kaimu Meneja  Uhusiano wa Bi. Leila Muhaji amewaomba radhi Wananchi kwa usumbufu uliojitokeza na kuwasisitiza kuwa sasa wanaweza kununua katika mifumo iliyozoeleka.

Bi. Muhaji amesema kuwa TANESCO inatambua umuhimu wa umeme hivyo   kuwataka watanzania kuwa na Imani na shirika lao kwani lipo kwa ajili ya kuwahudumia  kama inavyohitajika.




   Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania Tanesco, Leila Muhaji akifafanua jambo wakati wa Mkutano wake na Waandishi wa Habari juu ya kuimarika kwa Mfumo wa Ununuzi wa luku mara baada ya kuhamia sehemu nyingine. 


Waandishi wa habari habari walifika katika mkutano huo wakifatilia kwa Makini. --

No comments:

Post a Comment