December 21, 2017

BODI YA WAKURUGENZI TANESCO YATEMBELEA MIKOA YA KUSINI


Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ikiongozwa na Mwenyekiti wake Dk. Alexander Kyaruzi (Pichani anayesaini) na baadhi ya Viongozi Waandamizi wa TANESCO, imefanya ziara katika Mikoa ya Kusini.

Lengo la ziara ziara hiyo ni kukagua sambamba na kujionea kasi ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme inayoendelea katika Mikoa hiyo ikiwemo miradi ya kufua umeme na ile ya usafirishaji.

Aidha, ziara hiyo imetumika kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali za Wateja wa Shirika.



No comments:

Post a Comment