August 17, 2018

Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa akizungumza na waandishi wa habari kutangaza operesheni maalum ya wahalifu wa miundombinu ya umeme na maji.


Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa akizungumza na waandishi wa habari kutangaza operesheni maalum ya wahalifu wa miundombinu ya umeme na maji.
Dar es salaam.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam limezindua operesheni itakayowezesha kutokomeza wanaohujumu miundombinu ya maji na umeme.

Operesheni hiyo imezinduliwa leo Agosti 17, 2018 na Kamanda wa polisi Kanda Maalum Lazaro Mambosasa alipokutana na wadau kutoka shirika la umeme (TANESCO) pamoja na shirika la maji safi (DAWASCO)

Kamanda Mambosasa amesema siku zahivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la watu wanaojiunganishia miundombinu hiyo bila kufuata utaratibu na kuzisababishia hasara kampuni hizo

Kaimu Meneja uhusiano wa Tanesco Leila Muhaji amesema watashirikiana na jeshi la polisi kuhakikisha wote wanaohujumu miundombinu hiyo wanakamatwa.

 “Tutashirikiana na jeshi la polisi Kanda maalum kuhakikisha wote wanaohujumun miundombinu hii tunawakamata kwakuwa wamekuwa wakiliingizia shirika hasara hasa wanapoiba mafuta kwenye transfoma kwaajili ya kupikia”amesema Muhaji.

Ameongeza kuwa kwa sasa umeme unapatikana kwa urahisi kwenye maeneo yote na shirika linaende kusambaza umeme kwenye maeneo ambayo haujafika.

No comments:

Post a Comment