August 2, 2018

Rufiji Hydropower Project MW 2100 kuendesha treni ya umeme

Wazi Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani akifungua kikao hicho, kushoto ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ma kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba 

MOROGORO 

WAZIRI wa Nishati, Dk. Medard Kalemani, amesema kuwa umeme utakaozalishwa kwenye mradi wa Rufiji Hydropower Project  (Strigler’s Gorge)ndio utakaotumika katika uendeshaji wa treni ya kisasa ya umeme.

Kutokana na hali hiyo amesema kuwa Serikali itakikisha inasimamia kikamilifu utekelezaji wa mradi huo kwa wakati ili uweze kuleta manufaa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

Hayo aliyasema jana mjini Morogoro, alipokuwa akifungua kikao cha mawaziri, makatibu wakuu wa wizara na wataalamu mbalimbali zikiwamo Wizara 11 ambao wanatekeleza mradi huo.

Alisema mradi huo pindi utakapokamilika unatarajiwa kuzaliwa megawati 2,100 pindi utakapokamilika mwaka 2010.

 “Hivyo tumekutana hapa kujadili taarifa ya wataalamu kuhusu mradi, kutafakari changamoto na kuzifanyia kazi pamoja na kutembelea eneo la mradi.

“Hivi pamoja na hali hiyo kutakuwa na kazi ya kujenga transmi,” alisema Dk. Kalemani.
Kutokana na umuhimu mkubwa wa mradi huo kwa Taifa, Dk. Kalemani, alisema Serikali itachukua hatua za kisheria kwa yeyote atakayekwamisha uwetekelezaji wa mradi huo ambao utekelezaji wake unahusisha wizara 11 huku ukisimamiwa na Wizara ya Nishati kupitia Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).

Waziri huyo wa Nishati, alisema tangu ilipoasisiwa azma ya utekelezaji wa mradi huo na Rais Dk. John Magufuli, Julai mwaka jana Serikali kupitia Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na wizara nyingine walianza usimamizi wa haraka wa utekelezaji wake.
“Mradi huu utazalisha Megawati 2,100 ulibuniwa miaka mingi lakini ulichelewa kutekelezwa. Julai mwaka uliopita (2017) Rais Dk. John Magufuli aliweka wazi azma ya utekelezaji wa mradi huu.

“Waheshimiwa mawaziri na wajumbe mradi wa Mto Rufiji unaweza kuusema ni mradi rahisi sana kama miradi mingine lakini kwa historia ya uzalishaji wa umeme kwa nchi yetu huu utakuwa mradi mkubwa sana.

“Mradi mkubwa tuliona kwa sasa wenye megawati nyingi 240, ambao ni Kinyerezi namba mbili na katika miradi ya miradi ya maji ni wa megawati 204 kwa hiyo kuna kila namna ya kuongeza juhudi za kuukamilisha mradi huu. Nichukue nafasi hii kwa heshima kubwa kuipongeza Serikali hasa kupitia kwa Mheshimiwa Rais kwa kuamua kuutekeleza mradi huu nasi kama wasimamizi na watekelezaji wake tutatumia kila namna kila nguvu na akili tuliyonayo kuutekeleza kwa dhati mradi huu hadi ukamilike.

“Hatutasita kuchukua hatua kwa mtu yeyote mwenye nia ama ya kuuchelewesha ama kuukwamisha hatutasita kuchukua hatua za kisheria sisi tunaomba mradi huu ndio mkombozi pekee. Kama Serikali tumedhamiria kuutekeleza mradi huu na tumejipanga vizuri,” alisema
Alisema jambo la kwanza linalohitajika ni spidi ya utekelezaji kwa wataalamu na usahihi wa utekeleza wake pamoja na uweledi kwenye mradi huo.

Waziri huyo wa Nishati alisema
Alisema kwa sasa Serikali inaendelea kumtafuta mkandarasi ambaye atatekeleza mradi huo pamoja na msimamizi wa mkandarasi ambaye sharti apatikane kabla mkandaasi hajapatikana.

“Tunaendelea kutekeleza miradi ya kujenga miradi ya kujenga usafirishaji wa umeme huo (trasmision line)  ya kuutoa umeme huo Rufiji na kuupeleka hadi Chalinze ambapo umeme huu pia unautarajia sana utumike kuendesha treni mpya ya Standard Gauge inayoanza kutumika mara baada ya mradi kukamilika.

“Kwa hiyo huu ni mradi muhimu kwetu sisi Serikali maandalizi yanakwenda sawa ikiwamo kuanza kuona kuona kuanzia sasa namna ya utekelezaji wake,” alisema Dk. Kalemani

Kama mtakumbuka Bonde la Rufiji lilikuwa chini ya usimamizi wa RUBADA, lakini kwa kuwa wao walikuwa wakisimamia walishindwa kuutekeleza kutokana na kuwa wao si kazi yao kujenga umeme kwani lilikuwa jukumu la Tanesco.

“Mwaka jana tulipoanza mradi kuliwapo na changamoto za kawaida ikiwamo kujenga uelewa wa mradi huu. Hivyo ninapenda kusema kwamba taratibu za kumpata mkandarasi zinaendelea na kufikia Septemba mwaka huu atakuwa amepatikana. Kazi yetu sisi ni kuweka mazingira wezeshi kwa mkandarasi ili awezwe kuutekeleza mradi huu kwa wakati,” alisema Dk. Kalemani
Alisema lengo la mkutano huo utaangalia masuala matatu ambayo ni kupata taarifa ya utekelezaji na hatua za kuchukua, kutafakari changamoto za mradi na kutembelea eneo la mradi ili kuona hali halisi.

Dk. Kalemani, alisema ni vema kila mtaalamu kwa nafasi hasa waliohudhuria kwenye mkutano huo kutafakari kwa kina na hatua za kuchukua ili kuhakikisha utekelezaji unakamilika kwa wakati.
Alisema kwa sasa nchi ina Megawati 1582 baada ya kuongezewa uwezo wa mtambo wa umeme wa Kinyerezi II na mwishoni mwakani zitaingizwa megawati 185 kupitia mtambo wa Kinyerezi I.

“Lengo ni kufikisha megawati 500 hadi kufikia mwaka 2020 na ifikapo mwaka 2025 kuwa na megawati 10,000. Mradi huu tunaweza kusema ni rahisi lakini pia ni wa kihistoria na ndiyo mradi mkubwa kwetu. Na tutaukamilisha kama ulivyopangwa na serikali.

“kupitia mkutano huu utapata taarifa na mazingira wezeshi kwa kila mdau ili kuweza kuona wapi kuna changamoto na namna ya kuchukua ili twende haraka,” alisema

Waziri huyo wa Nishati, alisema kuwa kikao hicho cha mawaziri ni cha pili kufanyika ambapo cha kwanza kilifanyika Aprili mwaka huu.


Mkutano huu umehudhuriwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba pamoja na makatibu wakuu wa Wizara Malisili na Utalii, Ofisi ya Makamu wa Muungano na Mazingira, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Uchukuzi.






No comments:

Post a Comment