April 13, 2017

Makamu wa Rais:"siamini kwenye kushindwa, maji yatatiririka tu"



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha Wageni kituo cha kufua umeme cha Mtera



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akiwahutubia wadau mbalimbali alipotembelea Mtera



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Dkt. Tito E. Mwinuka.


 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa TANESCO



 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Kituo cha Mtera
Mhandisi John Skauki


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Hassan Suluhu akiongea katika ziara yake Kituo cha kufua umeme kwa njia ya maji cha Mtera alisema amezindua kikosi kazi cha kuokoa mfumo-ikolojia wa bonde la mto Ruaha Mkuu.
 
Akiwa katika ziara hiyo Mhe. Samia aliupongeza uongozi wa TANESCO na Wafanyakazi wa Kituo hicho kwa kazi kubwa wanayoifanya “Niwapongeze Mafundi na Uongozi kwa kujituma kuhakikisha tunapata umeme na kwa kufika hapa nimejionea hali halisi”. Alisema.

Kutokana na hali halisi ya uharibifu katika mto Ruaha Mkuu, kikosi kazi hicho kimehusisha Wizara Tano miongoni mwa hizo ni Wizara za Nishati na Madini, Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Wizara ya Nishati na Madini, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira.

Aliongeza kamati hiyo, itakapomaliza kazi itatoa mapendekezo Serikalini na Serikali itaangalia hatua za kuchukua na kipaumbele ili kuhakikisha maji yanatiririka katika mto huo “Tumeianza kazi ya kufufua ikolojia katika bonde la mto Ruaha Mkuu, siamini kwenye kushindwa, maji yatatiririka tu”. Alimalizia Mhe. Samia.

Awali akimkalibisha Mhe. Makamu wa Rais, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Tito E. Mwinuka, alimshukuru na kumpongeza Makamu wa Rais kwa juhudi zake za kulisimamia suala hili kwa kina na kuanzia kikosi kazi maalum cha kufanya utafiti wa namna ya kurejesha ikolojia mto Ruaha Mkuu.

Kwa upande wake Meneja wa Kituo cha kufua umeme Mhandisi John Skauki akitoa historia ya Mtera kwa kifupi kwa Makamu wa Rais alisema Kituo hicho kilijengwa katika awamu ya tatu ya Mradi wa Umeme Ruaha Mkuu (The Great Ruaha Power Project) ambapo Awamu ya Kwanza ilikuwa kati ya Mwaka 1970 hadi 1975, Bwawa dogo 125Mm3 Kidatu, Mgodi wa Kidatu, Mitambo miwili ya Megawati 50 kila mmoja.   


Awamu ya Pili ilikuwa kati ya Mwaka 1977 na 1981 ambapo mitambo miwili ya Megawati 50 kila mmoja iliwekwa Kidatu, Bwawa kubwa Mtera 3.7Bm3 na Awamu ya Tatu ilikuwa kati ya Mwaka 1984 na 1988 ilihusisha  Mgodi wa Mtera na Mitambo miwili ya Megawati 40.

Akielezea zaidi alisema ujenzi ulianza mwaka 1984 hadi 1988 na Gharama za mradi ni Dola za Kimarekani 1,580M na kuongeza mitambo imefungwa ndani ya mgodi wastani wa mita 100 chini ya ardhi na uwezo wa kuzalisha umeme kiasi cha Megawati 80 kwa mashine zote mbili, aidha Mtera inachangia asilimia 14.26 kwenye  mitambo ya  maji

Akitoataarifa ya ufuaji umeme alisema hutegemea kiasi cha maji yaliyopo bwawani, yanayotakiwa Kidatu na mahitaji ya umeme katika Gridi ya Taifa.
Utaratibu huu huongozwa na kituo cha kuendesha Gridi ya Taifa kilichopo Ubungo  Jijini Dar es Salaam (Ubungo Grid Control Centre).
 
“Maji huporomoka katika njia yake (Penstock) kina cha mita 92, huzungusha Gurudumu (Turbine) ambalo huzungusha Jenereta kwa kasi ya mizunguko 300 kwa dakika. Baada ya kuzungusha Gurudumu, maji hupita chini ya ardhi (tail race tunnel) umbali wa kilomita 11 na baadaye kurudia kwenye mkondo wake wa awali” alimalizia Mhandisi skauki.

Ziara hiyo ya Mhe. Makamu wa Rais ilijumuisha wadau mbalimbali wakiwemo Ujumbe kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Uongozi wa TANESCO na Wafanyakazi.

No comments:

Post a Comment