April 20, 2017

Kikosi kazi cha kuokoa mfumo wa ikolojia katika bonde la mto Ruaha Mkuu Chaanza kazi.




Kaimu Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Mhandisi Tito E. Mwinuka akitoa elimu kwa Wananchi wanaoishi katika vyanzo vya maji kuhusu umuhimu wa utunzaji wa mazingira

Na Henry Kilasila

Kikosi kazi hicho kilizinduliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan Mwezi Aprili Mwaka huu alipokuwa katika ziara Mkoani Iringa na kutembelea kituo cha kufua umeme kwa njia ya maji cha Mtera.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Dk. Tito E. Mwinuka, alisema Shirika la umeme Tanznaia (TANESCO) kama mdau muhimu linashiriki kikamilifu katika zoezi hili kwani Mto Ruaha Mkuu ni moja ya vyanzo vya maji yanayotumika katika ufuaji umeme katika vituo vya kufua umeme kwa njia ya maji.

 Aliongeza kuwa ufuaji umeme kwa njia ya maji ni nafuu zaidi ukilinganisha na Gesi, mafuta ama kununua kwani uzalishaji wa unit moja ni shilingi 36 ndio maana Serikali imekuwa na mipango endelevu ya  kuwa na vyanzo vingi zaidi.

Moja ya vyanzo vya umeme katika Gridi ya Taifa ni Ufuaji wa umeme kwa njia ya maji ambapo vyanzo hivyo vinachangia kwa 41% katika Gridi ya Taifa, Vituo hivyo ni Kidatu, Kihansi, Mtera, Pangani, Nyumba ya Mungu na Hale. 

Ufuaji wa umeme umekuwa ukiathirika Kutokana na hali halisi ya uharibifu katika vyanzo vya maji vinavyopeleka maji katika Bonde la mto Ruaha Mkuu kupungua ama kukaukaa, kikosi kazi hicho kimeanzan na vyanzo vya mto Mbukwa na mto Mtitafu vilivyopo Mkoani Njombe.

Uharibifu huo ni pamoja na shughuli za kilimo cha umwagiliji maarufu kama (vinyungu) unaofanyika kandokando mwa vyanzo vya maji, mabadiliko ya tabia ya Nchi yanayopelekea upungufu wa mvua, ufugaji wa mifugo na matumizi ya maji katika vyanzo hivyo  yameongezeka kutokana na ongezeko la Watu maeneo hayo.

Madhara makubwa yanatokea kipindi cha kiangazi ambapo Wakulima hufanya umwagiliaji kwa kutengeneza mifereji kuelekea katika mashamba yao, hivyo kusababisha maji kukauka mto Ruaha Mkuu.

Kitaalamu ndani ya mita sitini (60) kutoka vyanzo vya maji hapatakiwi kufanyika shughuli za kibinadamu, lakini zimekuwa zikifanyika ndani ya mita hizo,  hivyo imefika wakati hatua lazima zichukuliwe ili kuokoa hifadhi ya vyanzo vya maji na kurejesha uoto wa asili ili maji yaweze kupatikana mwaka mzima katika Bonde la mto Ruaha Mkuu.

TANESCO kwa kushirikiana na wadau wengine wametoa elimu kwa Wakulima ya namna ya kufanya kilimo kinachoendana na uhifadhi wa mazingira ikiwa ni pamoja na kutokufanya shughuli zakibinadamu ndani ya mita 60. 

Hatua nyingine zilizochukuliwa ni upandaji wa miti ambayo haikaushi maji na inayosaidia uboreshaji wa uoto wa asili na ukataji wa miti aina ya miwato iliyokuwa pembezoni mwa vyanzo vya maji ambayo inakausha maji. Zoezi hili la upandaji miti llifanyika Mwezi Februari Mwaka huu ambapo ilipandwa miti 2600.





mto Mbukwa ambao ni moja ya chanzo cha maji katika bonde ka mto Ruaha

 
Kikosi kazi kikiwa kazini






No comments:

Post a Comment