April 10, 2017

Dkt. Mwinuka: zoezi la ukataji umeme kwa wadaiwa ni endelevu


Mkurugenzi Mtendaji TANESCO, Dkt. Tito E. Mwinuka

Na Henry Kilasila

Mkurugenzi Mtendaji TANESCO, Dkt. Tito E. Mwinuka amesema zoezi linaloendelea la kukata umeme kwa wadaiwa sugu ni endelevu na amewataka wadaiwa kulipa Bili zao hasa katika kipindi hiki cha Siku kuu za Pasaka ili kuepuka usumbufu wa kusitishiwa Huduma ya Umeme.

Ametoa tahadhari hiyo, Aprili 10, 2017 Ofisini kwake Ubungo Jijini Dar es Salaam, aidha aliwashukuru Wateja ambao wameshaanza kilipa malimbikizo ya madeni yao, na ambao wamewekeana makubaliano ya kulipa madeni kwa awamu na TANESCO.
Aliongeza fedha Shirika linazowadai Wateja wake zinahitajika sana kuboresha miundombinu ya TANESCO.

Akiwa katika Mkutano huo na wana Habari, pia aliwataka Wateja na Wananchi kuwa waangalifu kipindi hiki cha mvua kwani hutokea uharibifu katika miundombinu ya Shirika kama kuanguka kwa nguzo ama nyaya kukatika na kuwataka kutoa taarifa TANESCO mara moja.

Aidha kwa Niaba ya Bodi ya Wakurugenzi, Menejimenti ya TANESCO na Wafanyakazi amewatakia Wananchi wote Heri ya Sikukuu ya Pasaka.

Mwanzoni mwa Mwezi Machi 2017, TANESCO ilitoa notisi ya siku kumi na nne kwa Wadaiwa ambao wamelimbikiza madeni ya umeme ambayo iliisha Machi 22, 2017, ikiwa ni kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ya kuitaka TANESCO kuwakatia umeme wadaiwa sugu.

Katika agizo hilo Mhe. Rais aliitaka TANESCO kukusanya madeni kwenye Taasisi zote inazozidai za Serikali na Binafsi ili kuliwezesha Shirika hili kutoa Huduma kwa ufanisi.


No comments:

Post a Comment