December 9, 2014

TAARIFA KWA WATEJA WA MAENEO YA UPANGA NA AZIKIWE

 Shirika la Umeme Tanesco linawatarifu wateja wake wa maeneo ya Upanga na mtaa wa Azikiwe kuwa kumetokea shoti kubwa muda wa saa 11.30jioni baada ya Mkandarasi wa mradi wa Hifab kukata waya mkubwa wa msongo wa kilovolti 11 na hivyo kusababisha Kituo cha Kupooza na Kusambaza Umeme cha Mjini Kati (City Centre) kuzima ghafla. Mafundi wa Karakana ya Umeme kutoka Makao Makuu wanashugulikia tatizo na tunatarajia umeme utarudi kesho mchana baada ya kuunga waya huo na kubadili vifaa vilivyoungua kwenye Kituo cha City Centre. Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza. Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano Tanesco Makao Makuu.

No comments:

Post a Comment