July 11, 2018

Dkt. Medard Kalemani azindua Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya III Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma



Waziri wa Nishati Dk. Medard Kalemani, akiambatana na  Viongozi wengine wa Serikali Wilayani Kasulu na Mkoa kigoma, amezindua mradi wa umeme Vijijini Awamu ya Tatu kwa Vijiji 149 vya Mkoa wa Kigoma.

Kwa Mkoa wa Kigoma uzinduzi huo umefanyika katika Kijiji cha Rusesa Wilayani Kasulu.

Katika uzinduzi huo Dkt. Kalemani alitoa maagizo kwa wasimamizi wa mradi huo kwa Wilaya nne ambazo zilichelewa kupata mradi huo na kuwataka wasimamizi TANESCO na Wakala wa Nishati Vijijini kuhakikisha wanamsimamia Mkandarasi ili ifikapo mwezi Juni, 2019 mradi uwe umekamilika.

Aidha, alitoa maagizo kwa Uongozi wa TANESCO Mkoa wa Kigoma kuanzisha Ofisi ndogo katika eneo la Rusesa kwa minajili ya kusikiliza kero za Wateja na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kwa gharama zilizoidhinishwa na Serikali.

Pia Dkt. Kalemani aliwasisitiza Wananchi kuhakikisha wanalinda miundombinu ya umeme kwani inagharimu pesa nyingi kujengwa"Niwaombe Wananchi muitunze miundombinu itakayojengwa kwa kuwa Serikali imetumia gharama kubwa sana kuwekeza katika miradi ya umeme". Alisisitiza.

Awali, akimkaribisha Mheshimiwa Waziri kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mkuu wa Wilaya ya Buhingwe na ambaye pia anakaimu Wilaya ya Kasulu Brigedia Jenerali Marco Gaguti alisemaWananchi wamekuwa wakiulizia kupatiwa huduma ya umeme mara kwa mara "Naamini uzinduzi huu utakuwa chachu kwa Wananchi kuanzisha Viwandavikubwa, vidogo na vya kati".






No comments:

Post a Comment