February 5, 2016

MKOA WA KINONDONI KASKAZINI




                                                     SHIRIKA LA UMEME TANZANIA
KATIZO LA  UMEME – MKOA WA KINONDONI KASKAZINI

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu wateja wake wa Mkoa wa Kinondoni Kaskazini kuwa kutakuwa na katizo la umeme kama ifuatavyo.

MUDA:          3:00  asubuhi hadi 10:00 jioni

TAREHE:      8 Februari, 2016 (JUMATATU)

SABABU:      Kuzimwa kwa laini ya BB5, kwa ajili ya kubadili nguzo zilizooza na nyaya zilizochakaa ili kudhibiti hali ya kukatika kwa umeme mara kwa mara,

MAENEO YATAKAYOATHIRIKA
Kunduchi yote, baadhi ya maeneo ya Salasala, Kilongawima na Mbezi beach, Recruitment Training School (RTS) of TPDF, Mbuyuni, MECCO, JKT machimbo, Tegeta darajani, Benaco, shule ya Green Acres, Majumba sita, Kinzudi pamoja na maeneo yanayozunguka.

TAREHE:      9 Februari, 2016 (JUMANNE)

SABABU:      Kuzimwa kwa laini ya MK 6, kwa ajili ya kubadili nguzo zilizooza na nyaya zilizochakaa ili kudhibiti hali ya kukatika kwa umeme mara kwa mara,

MAENEO YATAKAYOATHIRIKA NI:
Baadhi ya maeneo ya barabara ya Mwaya na Chole, mtaa wa Uganda, kota za bandari na UNDP, flati za NASAKO na IFM, Valahala na Baobao Village, hosteli za chuo cha Muhimbili, Kipepeo apartments, Sea cliff court, hoteli ya Alexander pamoja na maeneo yanayozunguka.

Tafadhali usishike wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka toa taarifa kupitia namba za simu zifuatazo: - Dawati la dharura Mkoa wa Kinondoni Kaskazini: 022 2701602, 0784 768584, 0716 768584 au namba za kituo cha miito ya simu 2194400 na 0768 985100

Uongozi unasikitika kwa usumbufu wowote utakaojitokeza


Imetolewa na:-         OFISI YA UHUSIANO,
                                    TANESCO – MAKAO MAKUU.


1 comment:

  1. Huku kimara kuja mbezi, hili tatizo la umeme limekuwa sugu week ya pili saivi. Tatizo lipo wapi? Na lini mambo yatakaa sawa.

    ReplyDelete