November 22, 2016

BANK OF AFRICA YASAINI MKATABA NA TAASISI YA AFD ILI KUWEZESHA UTOAJI WA MIKOPO YA UWEKEZAJI KATIKA NISHATI MBADALA

Kutoka kushoto ni Bw. Amishadai Owusu-Amoah Mkurugenzi Mtendaji wa BANK OF AFRICA-Tanzania akisaini mkataba na Bw. Bruno Deprince Mkurugenzi wa Kanda wa AFD Afrika Mashariki.

Kutoka kushoto ni Bw. Youssef Benrhafiane Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Mikopo na Udhibiti wa BANK OF AFRICA- Tanzania, Bw. Amishadai Owusu- Amoah Mkurugenzi Mtendaji wa BANK OF AFRICA- Tanzania, HE Malika Berak, Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Bw. Bruno Deprince Mkurugenzi wa Kanda wa AFD Afrika Mashariki na Bw. Thomas Richard, Mwakilishi wa Shirikisho la viwanda Tanzania.

Tanzania, 22nd Novemba 2016 –Agence Française de Développement (AFD) na BANK OF AFRICA- Tanzania leo wametia saini mkataba wa makubaliano ya kutoa mikopo kiasi cha shilingi bilioni 25.67 kusaidia uwekezaji kwenye nishati mbadala na ufanisi wa nishati.

Makubaliano hayo, yamewezesha upatikanaji wa zaidi ya dola milioni 11.84 kwa ajili ya kukopesha miradi mbalimbali iliyojikita katika nishati mbadala au kuongeza ufanisi wa upatikanaji au matumizi ya nishati hapa nchini kupitia BANK OF AFRICA.

Mkataba huo umesainiwa na ndugu Bruno Deprince ambaye ni Mkurugenzi wa Kanda wa AFD na ndugu Ammishaddai Owusu-Amoah, Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa BANK OF AFRICA, mbele ya Mheshimiwa Bi Malika Berak, Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Mheshimiwa Mikael Melin Programme, Meneja katika Ujumbe wa Umoja wa Ulaya kwa Tanzania na Mheshimiwa Thomas Richard, Mwakilishi wa Shirikisho la Viwanda nchini (CTI).

Katika makubaliano hayo, taasisi zote mbili zimethibitisha kushirikiana kupitia mpango wa SUNREF (Matumizi Endelevu ya Maliasili na Nishati). Mpango huu bunifu utaiwezesha BANK OF AFRICA kutoa mikopo ya muda mfupi na mrefu itakayowavutia sekta ya umma na binafsi kutekeleza miradi katika nishati mbadala na ufanisi wa nishati, ambayo imekuwa ikipata changamoto katika upatikanaji wa mikopo.

Mpango huu ubunifu itawezesha BANK OF AFRICA kutoa mikopo ya muda mfupi na mrefu klatika viwango vya riba nafuu kulinganisha na viwango vya kawaida vya kibiashara kwa lengo la kuwawezesha wateja katika sekta binafsi na umma, kuondokana na changamoto ya upatikanaji wa fedha za kutekeleza mpango wa nishati mbadala.

Mikopo hii inaambatana na msaada wa kiufundi unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya ili kuiunga mkono BANK OF AFRICA lakini pia kuiwezesha benki hiyo kuongeza uwekezaji katika miradi inayochochea ukijani.

Msaada wa kiufundi pia utatoa utaalamu kwa wawekezaji na waendelezaji wa miradi ili kuwajengea uwezo katika kuendeleza nishati mbadala na kuongeza ufanisi katika matumizi ya nishati. Msaada huu utajumuisha maeneo yote ya uwekezaji kama maandalizi ya mradi, mchakato mzima wa uwekezaji pamoja na kujengewa uwezo wa kibenki.

Kwa upande wa Afrika Mashariki, SUNREF, inakuza mpango wa matumizi ya nishati zinazotoa gesi chafu kidogo kwa kugharimia uendelezaji wa miradi ya nishati mbadala na ufanisi katika matumizi ya nishati.

AFD inazisaidia benki za ndani katika kutambua fursa za uwekezaji katika nishati mbadala na kutoa mikopo inayochochea hali ya kijani pamoja na kutengeneza utaratibu mzuri wa ulipaji wa mikopo hiyo unaziofaa pande husika.

Programu hii imeundwa ili kuzisaidia biashara ziweze kutumia fursa ya mabadiliko ya hali ya hewa, pamoja na kuimarisha sekta ya benki kufadhili nishati mbadala na ufanisi wa nishati. Miradi ya nishati mbadala ni ile inayozalisha aina yoyote ya nishati (joto, mvuke, nguvu) bila kutoa nishati yoyote ya mafuta au chanzo chochote cha mionzi, ikiwa ni pamoja na nishati ya upepo na nishati ya jua.

Mradi huu utachangia pia kuongeza ufanisi wa nishati na mchango wa nishati mbadala katika ukuaji wa uchumi nchini,na hivyo kuchangia kupunguza uzalishaji wa gesi ya kaboni. Mradi huu pia utaziwezesha taasisi na biashara za kitanzania kupata teknolojia ya kijani pamoja na kuboresha ufanisi wao na ushindani wa jumla pamoja kuendeleza nishati safi.

Mkakati wa AFD umejikita katika kusaidia maendeleo endelevu ya kimazingira kupitia kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa kwa kutumia nishati zinazotoa gesi kidogo ya kaboni. Hii ni pamoja na, miongoni mwa mambo mengine, kuboresha ufanisi wa nishati, kupanua matumizi ya vyanzo vya nishati safi, na kupunguza uzalishaji wa gesi chafu.

No comments:

Post a Comment