January 2, 2018

Mhe. Mgalu akagua maendeleo ya ubomoaji jengo la TANESCO Makao Makuu


Naibu Waziri Nishati Mhe. Subira Mgalu, amekagua maendeleo ya ubomoaji wa jengo la TANESCO Makao Makuu ambapo ameridhishwa na hatua zinazoendelea.

Akielezea hatua za ubomoaji kwa Mhe. Naibu Waziri, Meneja Miradi Mhandisi Emmanuel Manirabona alisema suala la ubomoaji jengo lilianza kutekelezwa Novemba 17, 2017 baada ya kupewa notisi ya siku thelathini, ambapo Novemba 26, 2017 Wizara ilitembelea ili kukagua hatua zilizokwisha fikiwa katika utekelezaji wa zoezi hilo.

Aliongeza kati ya Novemba 27 na Desemba 06, 2017 zilifanyika kazi za kuondoa fanicha katika jengo linalobomolewa, pamoja na ubomoaji wa majengo ambayo sio ya ghorofa.

Desemba 4 hadi Desemba 10, 2017 ilifanyika kazi ya kuondoa mifumo (Miundombinu) ya TEHAMA.

Aidha, alifafanua kuchelewa kwa ubomoaji kumetokana na changamoto mbalimbali ikiwemo kupatikana kwa vifaa sahihi vya kubomolea.

Akielezea utekelezaji wa mradi alisema,  ubomoaji ghorofa ya tisa umekamilika na inatarajiwa jengo zima kukamilika Januari 11, 2018.





No comments:

Post a Comment