January 29, 2018

Mhe. Mgalu akagua Miradi ya REA Mkoani Kilimanjaro


Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Subira Mgalu amekagua utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini Awamu ya Pili na Tatu (REA PHASE II & III) Mkoani Kilimanjaro wenye jumla ya Vijiji 18 katika Wilaya za Rombo, Mwanga na Same.

Aidha, Mhe. Mgalu alitumia ziara hiyo kuwatambulisha Wakandarasi kwa Wananchi na kuwataka kutokurudia makosa yaliyojitokeza awali na kuhakikisha wanakamilisha kazi ndani ya muda uliopangwa.

Pia alitembelea Bwawa la kuzalisha umeme la Nyumba ya Mungu kujioneo shughuli za uzalisha.

Mhe. Mgalu alikamilisha ziara hiyo Mkoani Kilimanjaro Januari 26, 2018.







 





No comments:

Post a Comment