January 25, 2018

TANESCO yaboresha Huduma kupitia Mfumo mpya wa GIS


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeendelea kuboresha huduma zake kwa Wateja kwa kubuni na kuanzisha mfumo mpya wa kiteknolojia utakaokusanya na kujumuisha taarifa zotemuhimu za miundombinu ya umeme na Wateja kupitia mfumo wa GIS (Geographical Information System).

Mfumo huu unaambatana na ramani ya miundombinu ya umeme na makazi ya Wateja, ambao kwa kiasi kikubwa utasaidia Wataalamu na kutoa huduma kwa muda mfupi na kwa haraka zaidi.


No comments:

Post a Comment