January 10, 2018

TANESCO yawashukuru Wateja kwa mchango mkubwa mwaka 2017


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Dkt. Tito E. Mwinuka amewashukuru Wateja, wanahabari na wadau wote kutokana na mchango mkubwa kwa Shirika ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa ambazo zimeisaidia TANESCO katika kuboresha huduma zake.

Aidha, amesema hali ya uzalishaji umeme unaendelea vizuri kutokana na kuanza kufanya kazi kwa mashine mbili kutoka kituo cha kuzalisha umeme cha Kinyerezi II, kukamilika kwa ukarabati wa mashine ya kufua umeme Kidatu, na kuongezeka kwa kina cha maji kwenye bwawa la Mtera, kuimarika huku kumepelekea TANESCO kuwa na umeme wa ziada.

Akizungumzia njia za kusafirisha umeme, alisema ukarabati wa miundombinu unaendelea katika njia za kusafirisha umeme.

“Suala la kukatika kwa umeme Kigamboni, ufumbuzi wake utapatikana baada ya kukamilika kwa mradi wa njia ya kusafirisha umeme wa kilovolti 132 ambapo njia hiyo imefika kituo kipya cha Mbagala”. Alisema Dkt. Mwinuka.

Aliongeza hivi sasa Kigamboni inatumia umeme kutoka njia ya umeme ya kilovolti 32 ya Kipawa – Chang’ombe ambayo pia inatumiwa na Viwanda.

Alisema, licha ya mvua kuwa na changamoto ya uharibifu wa miundombinu ya umeme lakini inafaida kwa TANESCO katika mabwawa kwani inachangia asilimia 41.5.

No comments:

Post a Comment