November 28, 2013

TAARIFA KWA UMMA


MRADI WA UJENZI WA NJIA YA USAFIRISHAJI WA UMEME WA MSONGO WA KILOVOTI 220 KUTOKA SOMANGA MTAMA MPAKA KINYEREZI
ULIPAJI WA FIDIA KWA WAHANGA WANAOPITIWA NA MRADI
Kilwa Energy kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wana mpango wa kujenga njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 220 kutoka Somanga Mtama mpaka Kinyerezi.
Wananchi waliopitiwa na Mradi huu wanaombwa kurejea tangazo lililotolewa tarehe 01-08-2013 kwenye magazeti mbalimbali kuhusu ulipwaji wa fidia na kwamba malipo ya fidia yalitarajiwa kuanza kulipwa tarehe 30-11-2013. Kutokana na sababu mbalimbali tunasikitika kutoa taarifa kuwa zoezi hilo halitaanza kama lilivyotarajiwa.
Katika kipindi hicho baadhi ya mikataba muhimu inayohitajika kati ya Kilwa Energy, Serikali, na TANESCO ilikamilika na pia kukamilisha makabrasha ya fidia. Kwa sasa Kilwa Energy imetuma maombi serikalini kuomba kukamilisha mikataba yote iliyosalia na pia wanawasiliana na wafadhili mbalimbali kuona uwezekano wa kukamilisha mikataba hiyo mapema iwezekanavyo.
Zoezi la kuhakiki majina na ufunguzi wa akaunti ulisitishwa ili taratibu za mikataba iliyosalia ikamilike.
Ili kuokoa muda na kuharakisha zoezi zima wakati utaratibu wa kukamilisha mikataba unaendelea, Kilwa Energy na TANESCO wataendelea na zoezi la
1.     Kuhakiki majina ya wananchi wote wanaopitiwa na mradi kwa kupiga picha na kujaza fomu maalum itakayokuwa inaonesha malipo stahiki.
Wananchi watajulishwa lini zoezi la ulipaji fidia litaanza kupitia vyombo vya habari.
Kilwa Energy na TANESCO linawaomba tena wananchi wote wanaopitiwa na Mradi huu kuwa wavumilivu wakati huu wa ukamilishaji wa mikataba iliyobaki. Hivyo basi, tunatarajia mara tu mikataba hiyo itakapokamilika malipo yatashughulikiwa.
Kilwa Energy na TANESCO wanaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
IMETOLEWA KWA USHIRIKIANO WA WAKURUGENZI WATENDAJI WA KILWA ENERGY NA TANESCO

2 comments:

  1. Mimi ni mhanga Wa mradi huu na ningependa kujua lini hasa fidia italipwa?

    ReplyDelete
  2. suala hili limekuwa la muda mrefu sana na hatujuia litakwisha lini. Naomba kujulishwa hatua iliyofikiwa ikiwa ni pamoja na lini malipo yetu yatafanyika? Mimi ni mmoja wa wahanga wa mradi huo.Nashauri taarifa zitolewe kupitia vyombo vya habari na sio kukaa kimya.

    ReplyDelete