March 5, 2012

TANESCO na JICA waimalisha ushirikiano


         Wakarabati kituo kidogo cha kupoza umeme cha Ilala kwa pamoja.
 
Naibu Mkurugenzi wa TANESCO Usafirishaji
 Mwandisi Decklan Muhaki, akijadili jambo na  
Mmoja wa Wataalamu toka JICA
JICA, wakala wa Japan katika kusaidia nchi za Afrika katika kuzijengea uwezo kimaendeleo. Imekuwa na ushirikiano mzuri na Shirika la  Umeme Tanzania (TANESCO), Ambapo wamekuwa wakilisaidia shirika la TANESCO katika kuwajengea uwezo wataalamu wake  katika kuboresha utendaji kazi wao.

JICA wamesaidia katika kuboresha mitaala ya masomo katika chuo cha Tanesco, ambacho kinatoa mafunzo ya kujiendeleza kwa mafundi Mchundo na Wahandisi.
Tarehe 25 na 26 mwazi uliopita JICA wakishirikiana na TANESCO walifanya ukarabati kituo kidogo cha kupoza na umeme cha Ilala na kupita njia zote za kusambazia umeme zinazotokea katika kituo hicho ili kurekebisha na kuweka sawa, hii ilikuwa katika kutatua matatizo ya dhararu ya kukatika umeme yanayotokana na uchakavu wa miundombinu ya umeme.


Mafundi wa TANESCO na JICA wakiwa katika kazi 
ya pamoja
katika kituo cha kupoza umeme cha Ilala

1 comment:

  1. Mimi ni mkazi wa Dar eneo la moshibaa kwa Diwani. Sass ni zaidi ya siku 7 tunapata shida ya umeme Kupatwa mara kwa Mara kwa siku moja zaidi ya mara tatu. Pia umeme unaporudishwa unakuwa unaanza sana na kuwa na madhara ya aina mbili 1. Kuunguza vifaa Mimi king'amuzi, TV na pump ya maji vimeathirika

    ReplyDelete