March 2, 2012

TANESCO yafanikiwa kukamilisha ahadi ya Rais,kwa kufikisha umeme Mabwepande



Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Badra Masoud alipotembelea 
Makazi ya waathirika wa Mafuriko , Mabwepande.
Hatimaye Tanesco imekuwa taasisi ya kwanza kumaliza kuweka miundombinu mipya ya umeme kwa waathirika wa mafuriko waliopewa makazi mapya Mabwepande. Kufuatia janga la mafuriko lilitokea sehemu kadhaa za viunga vya Mji wa Dar Es Salaam na Serikali kuamua kuwahamishia wakazi wote waliokuwa katika maeneo hayo hatari kwa kuwapatia maeneo nje kidogo ya mji, Mabwepande kuwa makazi yao mapya na ya kudumu.

Kufuatia uzito wa tatizo ili Mh. Rais Jakaya Kikwete alikutana na wawakilisha wa taasisi muhimu za Serikali kuona jinsi ya kujenga miundombinu haraka katika maeneo ya Mabwepande ili waathirika waweze kuishi maisha salama na ya kawaida. TANESCO ikiwakilishwa na Meneja Mahusiano Bi, Badra Masoud.

Tarehe 13 Januari, Rais aliomba Taasisi zote zilizotakiwa kujenda miundombino kama Maji, Barabara na Umeme, kutoa ahadi ya lini watafikisha huduma hizo za dharura. Meneja Mahusiano Tanesco,Bi. Badra Masoud ambaye alimwakilisha,Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mwandisi William Mhando, kwakutambua umuhimu wa huduma ya umeme kwa waathirika, , alitoa ahadi ya siki 14 kumaliza kuweka miundombinu ya umeme.  Kikosi maalumu cha kukarabati umeme Dar es Salaam (KAUDA) walikabidhiwa jukumu ilo.

KAUDA baada ya kukabidhiwa ramani ya ujenzi wa makazi hayo, tarehe 16 walianza kazi rasmi ya kuweka miundombinu ya umeme. Kwasababu ya ukubwa wa eneo na uharaka wa mradi huu, ulifanya kazi ya ujenzi kuwa ngumu sana na kuwafanya KAUDA kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha wanatimiza ahadi ya kufikisha umeme kwa siku 14 tu.

Hatimaye tarehe 05, Feb Tumeweza kufikisha umeme kwenye viunga vyote vya makazi mapya ya Mabwepande. Meneja Mahusiano, Bi. Badra Masoud ametembelea maeneo ya ujenzi wa mradi na kushuhudia ujenzi umekwisha na taa chache zilizowekwa kwenye nguzo zikiwaka.

Badra Masoud akionyesha mwenye furaha kubwa, aliwapongeza  mafundi wa kikosi maalumu cha Tanesco (KAUDA), kwa kazi nzuri.



Transifoma inayopoza umeme tayari kwa kugawa umeme, 
na Taa kubwa kusaidia kangaza makazi

Nyie ni kikosi chetu cha kujivunia, nawashukuru sana kwa kazi nzuri, natambua ugumu wa kazi hii, hata nilipokuwa natoa ahadi mwenyewe nilitia shaka lakini niseme mumetupa heshima kubwa kama shirika”

“TANESCO INAYAANGAZA MAISHA YAKO”




No comments:

Post a Comment