March 23, 2012

Balozi wa Japan nchini atembelea Chuo Cha TANESCO Masaki

Balozi wa Japan Mr. Masaki Akodo, akielezea jambo, Chuo Cha TANESCO jana.

Balozi wa Japan nchini Bw. Masaki Okoda, Machi 22, 2012 ametembelea  Chuo Cha TANESCO, kilichopo Masaki Jijini Dar es Salaam ikiwa ni ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi inayofadhiliwa na Shirika la Ushirikiano la Kimataifa la Japan  (JICA).  JICA wamekuwa wakishirikiana na chuo hicho katika kuandaa mitaala na pia wamekuwa wakilisaidia Shirika la umeme Tanzania  (TANESCO) kwa ushauri katika masuala ya ufundi na teknolojia.

Ujumbe wa Balozi Okoda uliongozwa na mwakilishi wa JICA Tanzania, Bi. Minako Yamanoto na Balozi Mdogo wa Japan nchini Mr. Yukinori Seki. Ujumbe huu ulipokelewa na Mkuu wa Chuo  cha TANESCO, Bi. Subira Wandiba na Meneja Mwajiri na Mahusiano sehemu ya kazi TANESCO, Bw. Ahmed  Mnunguye pamoja na uongozi mzima wa Chuo hicho.

Mkuu wa Chuo Bi. Subira Wandiba, alimweleza Balozi, Masaki Okoda, kwamba chuo chake kinatoa kozi za kiufundi kwa mafundi mchundo na wanategemea siku za karibuni kuanza kutoa kozi kwa wahandisi ambao watakuwa na madarasa yao katika Chuo kingine kam hicho ambacho kimejengwa katikati ya jiji eneo la Stesheni, pia alisema lengo la chuo ni kuwajengea uwezo  wafanyakazi wa TANESCO ili kuboresha utendajikazi wao  na kwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia.

Kwa upande wake balozi Okoda, alipata nafasi ya kuuliza maswali mengi hasa akitaka kujua tofauti ya ya kiutendaji kati ya wahandisi na mafundi mchundo, pia akitaka kujua jinsi gani chuo hicho kinaweza kusaidia katika utatuzi wa tatizo la uchakavu wa miundombinu na baadae alitembelea maeneo mbalimbali ya chuo hicho kuona mazingira pamoja na kukutana na wanafunzi waliokuwa katika masomo kwa vitendo. Wanafunzi hao walikuwa wanajenga njia mpya za mfumo wa kusafirishia umeme.


Akiaagana na Uongozi wa Chuo Balozi Okoda, aliwapongeza JICA na uongozi wa Chuo kwa kazi nzuri na kuwashauri kuona jinsi ya kupata eneo kubwa zaidi kwa ajili ya kukiendeleza, hii ni baada ya kuona eneo la chuo ni dogo akilinganisha na mipango mizuri na mikubwa ya chuo. 

 Habari katika picha

Mkuu wa Chuo cha TANESCO, Bi. Subira Wandiba akielezea jambo.

Mhandisi.Msemwa wa (kwanza kulia) akiwaelezea jambo, Balozi Masaki na Mr. Jiro.





Japanese ambassador pays a visit to TANESCO Training School

Bi.Fridah Nizamadin toka Dodoma, akiwa juu ya nguzo katika mafunzo ya vitendo.
Japanese ambassador to Tanzania Mr Masaki Okoda on March 22, 2012 paid an official visit to TANESCO Technical Training School (TTTS) at Masaki in Dar es Salaam to look over as one of the JICA funded projects.
JICA has cooperated with (TTTS) in formulation of curriculums for students at the school and has extended consultancy support services on technical and technological issues to TANESCO.
The Okoda’s visit was headed by JICA (T) representative Ms Minako Yamanoto and second Japanese ambassador to Tanzania Mr Yukinori Seki.



The delegation was time-honored by TTTS head Ms Subira Wandiba, Manager Employees and labour Relations Mr Ahmed Mnunguye and the TTTS management.

The School’s head Ms Wandiba notified ambassador Okoda that school provides training to artisans and the plan is to train engineers in the near future at its newly established School in the City Centre close to railway station.
However Ms Wandiba insisted that the School targets at TANESCO employees capacity building, performance and technology improvement.

Responding to TTTS briefing, Mr Okoda asked the differences that exist between artisans and engineers in term of their duties, and finally asked how TTTS provides assistance to tackle the current old and overloaded TANESCO  infrastructures.
Later Mr Okoda had a chance to see practical training programme for construction of transmission line which was been carried by students at the site.
Before his departure Mr Okoda, congratulated TTTS management for the job well done and advised it to acquire more space to develop the school following huge and good plans underway.




No comments:

Post a Comment