March 12, 2012

Tunaomba radhi kwa wateja wetu wa Upanga na Katikati ya Mji (CITY CENTRE)


Hii ndio Transifoma iliyoharibika
Shirika la Umeme Tanzania – TANESCO linapenda kuwaomba radhi wateja wake wote wanaoishi maeneo ya Upanga Mashariki, Eneo la Sea View ,Eneo la kituo cha polisi Daraja la Salender  ,Hospitali ya  Agakhan ,  Mtaa wa  Azikiwe, Mtaa wa Mkwepu, Mtaa wa Makunganya, Bilicana Club, Maeneo yaliyoko kando kando ya barabara ya  Bibi Titi, Mahakama ya Kisutu ,Maktaba kuu ya Tanganyika, NSSF, DIT-Chuo cha ufundi, Upanga Magharibi, Maeneo ya ofisi za zima moto, Diamond Jubilee,Hospitali ya  Tumaini , JWTZ Upanga,Hoteli ya  Movenpik Serena , Barcklays House na maeneo yanayoizunguka kwa tatizo la kukosa umeme kuanzia tarehe 06/03/2012 jioni   hadi tarehe 9/03/2012 kutokana na kuharibika kwa transfoma kubwa iliyopo katika kituo chetu cha City Centre cha kusambazia umeme kwenye maeneo hayo kilichopo mkabala na  mahakama ya kisutu.

Kazi ya dharura ya kurejesha umeme maeneo hayo ilikamilika tarehe 09/03/2012 majira ya saa tisa usiku.
                                                                                                 
Uongozi wa mkoa wa Ilala pamoja na uongozi wa Shirika kwa ujumla unaomba radhi na kuwapa pole wateja wote kwa usumbufu wote walioupata kutokana na tatizo hili.

Kwa msaada na  matukio ya dharura tafadhali piga simu namba :
022 213 3330, 0784 768586, 0715 768586 ofisi ya mkoa Ilala, 0715 76 85 84 au 0688 00 10 71 ofisi ya wilaya ya Gongo la Mboto, 0684 00 10 68 ofisi ya wilaya ya Tabata na 0684 001066 ofisi ya wilaya ya viwandani. Nama za kituo cha huduma kwa wateja( Call centre numbers) 2194400 au 0768 985 100

Imetolewa naOfisi ya Uhusiano
TANESCO
Makao Makuu.

1 comment:

  1. Pamoja na jitihada zenu, tunawaomba muangalie kwanini umeme haupo stable yaani kua low voltage na high kila dakika tano hivi. Vifaa vinaweza kuharibika.

    ReplyDelete