December 10, 2013

KATIZO LA UMEME – MKOA WA ILALA



Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake wa Mkoa wa Ilala na Pwani kuwa Kutakuwa na Katizo la Umeme siku ya JUMATANO tarehe 11/12/2013 kuanzia saa 03:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni.  Sababu ni kufunga kifaa cha umeme kwenye njia ya Msongo mkubwa wa umeme ya Kipawa  na kukata matawi ya miti yaliyoizonga njia hiyo.

MAENEO YATAKAYOATHIRIKA:
Maeneo yote ya Kisarawe,Kiwanda cha Namera,JWTZ Gongo la Mboto, ulongoni,
Mongo la Ndege, Ukonga, kitunda, FFU na maeneo mengine yanayozunguka.

Tafadhali usishike waya uliokatika toa taarifa kupitia simu zifuatazo: Huduma za Dharua TANESCO Ilala 022 213 3330, 0784 768586,0715768586 Kituo chetu cha Miito ya Simu ( Call centre numbers) TANESCO MAKAO MAKUU 022-2194400 au 0768 985 100

Uongozi unasikitika kwa usumbufu wowote uliojitokeza


Imetolewa na:          OFISI YA UHUSIANO,
                                    TANESCO – MAKAO MAKUU.

No comments:

Post a Comment