September 17, 2016

MKURUGENZI MTEDAJI TANESCO AMPA POLE MKUU WA MKOA KAGERA




 Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali (mstaafu), Salum Kijuu, (kushoto), akimkaribisha ofisini kwake, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), Mhandisi Felchesmi Mramba, alipomtembelea Septemba 17, 2016 ofisini kwake mkoani humo ili kumpa pole kufuatia athari za tetemeko la ardhi
 Mkuu wa Mkoa, Meja Jenerali (mstaafu), Salum Kijuu, akitoa taarifa za athari hizo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Felchesmi Mramba na ujumbe wake

 Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali (mstaafu), Salum Kijuu, akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Felchesmi Mramba na ujumbe wake, mara baada ya mazungumzo yao, Septemba 17, 2016
 Meja Jenerali Kijuu, akiagana na Mhandisi Mramba na ujumbe wake



  Fundi wa TANESCO mkoani Kagera, akiondoa nyaya za umeme baada ya kukata umeme kwenye nyumba moja eneo la Hamugembe, ikiwa ni hatua ya kuchukua tahadhari
 Mhandisi Mramba, akitembelea maeneo yaliyoathirika na tetemeko hilo huko Hamugembe
  Mhandisi Mramba, akiongea na waanishi wa habari kwenye eneo moja lililoathirika vibaya na tetemeko la ardhi huko Hamugembe
  Bi Slivia Philip, akiwa ameketi nje ya nyumba yake iliyoharibiwa vibaya na tetemeko eneo la Hamugembe-Mkishenyi mkoani Kagera, Septemba 17, 2016

  Violet Anaclet, mkazi wa Hamugembe-Mkishenyi, akiwa na mawazo wakati akijipumzika kwenye eneo la wazi baada ya nyumba aliyokuwa akiishi kuharibiwa na tetemeko, Septemba 17, 2016

  Mhandisi Mramba, akisalimiana na Afisa Mtendaji wa Kata ya Hamugembe, Sudi Ahmada, Septemba 17, 2016
  Kaimu Meneja wa TANESCO Kanda ya Ziwa, Mhandisi Kalisa, (kulia), akizungumza na fomeni wa genge la TANESCO Kanda ya Ziwa, Freddy Lusama, wakati Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO Mhandisi Mramba alipowatembelea wafanyakazi wa Shirika hilo waliokuwa wakiendelea na kazi kwenye eneo la Hamugembe mkoani Kagera, Septemba 17, 2016
  Meneja wa TANESCO mkoani Kagera, Mhandisi Francis Maze, (katikati), akiwa amezungukwa na wafanyakazi wa shirika hilo akiwapa maelekezo, Septemba 17, 2016


  Mhandisi Mramba, alipofika eneo la Hamugembe, kuona jinsi wafanyakazi wa Shirika hilo wakiendelea na kazi

 Kwa bahati nzuri hakuna nguzo za umeme zilizoathirika na tetemeko hilo, hata hivyo TANESCO imeamua kuchukua tahadhari kwa kukagua ili kuona kama kuna nguzo yoyote iliyoathirika na kuchukua hatua za kubadilisha, kama ambavyo lori hili lililoonekana maeneo ya Hamugembe likiwa na nguzo hizo
 Genizora Magili, anayehusika na masuala ya nyaya za umeme, akiwa amebeba vifaa vya kazi

  Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania, 9TANESCO), Leila Muhaji, akitoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya kiusalama ambayo wananchi wanapaswa kuzingatia pindi waonapo nyaya zilizoanguka au kutilia shaka yoyote kuhusiana na miundombinu ya Shirika



Na Henry Kilasila 

Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Mhandisi Felchesmi Mramba amemtembelea Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe Meja Jenerali (mstaafu), Salum Kijuu, Ofisini kwake.

Awali Mkuu wa Mkoa Kagera Meja Jenerali (mstaafu), Salum Kijuu, Akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji na ujumbe wake alielezea athari, uharibifu na maafa yaliyosababishwa na tetemeko lililotokea Jumamosi ya Septemba 10, 2016.

“Nawapongeza TANESCO pamoja na tetemeko hili miundombinu yao haikuleta athari kwa wananchi, hakuna vifo vilivyotokana na umeme” 

Aliongeza Mkoa umekuwa ukipokea misaada kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu na wadau mbalimbali kama madawa, vyakula, vifaa vya ujenzi maturubai.

“Tetemeko hili lilianzia sehemu za Misenyi na limesababisha uharibifu wa majengo takribani 200, vifo 17, majeruhi 253 kati ya hao wamebaki majeruhi 43 huku 23 kati ya 43 wakihitaji huduma ya upasuaji”. Alisema
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji Mhandisi Felchesmi Mramba kwa niaba ya TANESCO alimhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Kagera kwamba hakuna madhara yoyote kwenye miundombinu ya umeme na  ipo salama.

Eidha TANESCO imeshiriki kikamilifu kupitia Ofisi ya msajili wa Hazina, pia wafanyakazi wanajikusanya mmoja mmoja ili kuweza kuchangia.

“Tumetoa maagizo kwa mafundi wetu kufanya kazi masaa ishirini na nne, pia tumeongeza nguvu kutoka Mikoa ya Mwanza, Geita na Mara pamoja na Wilaya za jirani ambazo hazikupata madhara”. Alisema Mhandisi Mramba
Mhandisi Mramba alimuhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa upatikanaji wa umeme Mkoani Kagera utakuwepo bila shaka yoyote isipokuwa tu kwenye maeneo ambayo nyumba zimeathirika vibaya ili kuepusha athari zozote zinazoweza kutokea kutokana na kuguswa kwa nyaya za umeme.

No comments:

Post a Comment