September 13, 2013

KATIZO LA UMEME – MKOA WA MOROGORO



Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linasikitika kuwaarifu wateja wake wa Mkoa wa Morogoro kuwa kutakuwa na katizo la umeme kama ifuatavyo:-

TAREHE:      Jumapili Septemba 15, 2013

MUDA:           Saa 3:00asubuhi hadi Saa 12:00jioni

SABABU: -
Kufanya matengenezo ya tahadhari kwenye Transfoma namba 1 ya Msongo Mkubwa wa kilovolti 220, 132 na 33 ili kuzuia mafuta yanayovuja na kufanya marekebisho makubwa kwenye switchi ya msongo wa kilovolti 33.

NIA:-
Kuzuia katizo la ghafla la umeme linaloweza kutokea wakati wowote na kusababisha uharibifu wa vifaa vya umeme kwenye mfumo.

MAENEO YATAKAYOATHIRIKA:-
Maeneo yatakayoathirika ni Mkoa wote wa Morogoro

Tafadhali usishike au kukanyaga waya wowote uliodondoka, Toa taarifa Ofisi yoyote ya TANESCO iliyokaribu nawe au tupigie simu ya Kituo cha Miito na Huduma kwa Wateja namba 2194400 au 0768 985100



IMETOLEWA NA:   OFISI YA UHUSIANO,
TANESCO MAKAO MAKUU.

No comments:

Post a Comment