October 11, 2013

BAGAMOYO

KUOMBA RADHI
Shirika la Umeme Tanzania TANESCO linaomba radhi wateja wake wa Bagamoyo kwa katizo la umeme lililotokea kuanzia siku ya Jumapili Oktoba 6,  2013 saa 7:30 mchana hadi Jumatano Oktoba 9,  2013 saa 5:25 usiku kutokana na kuharibika kwa transfoma kubwa la MVA 2.5 ya msongo wa kilovoti 33/11 iliyopo Mwanamakuka.
Transfoma mbovu imeondolewa na kuwekwa nyingine ya MVA 7.5 na umeme sasa unapatika wa kutosha.
Shirika linasikitika sana kwa usumbufu wowote uliojitokeza katika kipindi chote cha tatizo hili.
Imetolewa na:   
Ofisi ya Uhusiano,
TANESCO Makao Makuu.                                 

No comments:

Post a Comment