October 17, 2013

MKOA WA ILALA



Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linasikitika kuwataarifu wateja wake wa Mkoa wa Ilala  kuwa kutakuwa na katizo la umeme kama ifuatavyo:-
TAREHE:    19/10/2013; Jumamosi
SAA:             3:00 Asubuhi-11:00 Jioni
SABABU:  Kubadilisha Nguzo Zilizooza, Kufanya Matengenezo na Kukata matawi ya Miti Katika Njia ya Umeme ya Msongo mkubwa wa Umeme wa Kariakoo.
MAENEO YATAKAYOATHIRIKA:
Hospitali ya Mnazi Mmoja na maeneo ya jirani, Benki ya Mkoa Dar-Es salaam (Dar-Es-Salaam Community Bank), Hoteli ya Peakock, Baadhi ya maeneo ya Mtaa wa Uhuru na Livingstone, Baadhi ya maeneo ya Mtaa wa Uhuru na Lumumba.
Tafadhali usishike waya uliokatika, toa taarifa upesi kupitia simu zifuatazo:
022 213 3330, 0784 768586, au Call centre namba 2194400 au 0768 985 100
Uongozi unasikitika kwa usumbufu wowote utakaojitokeza
Imetolewa na:   OFISI YA UHUSIANO,
TANESCO – MAKAO MAKUU.

No comments:

Post a Comment