October 11, 2013

KINONDONI

TAARIFA YA KATIZO LA UMEME MKOA WA KINONDONI KUSINI
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linasikitika kuwataarifu wateja wake wa Mkoa wa Kinondoni Kusini  kuwa kutakuwa na katizo la umeme siku ya JUMAMOSI tarehe 12/10/2013 kuanzia saa 3:00 Asubuhi hadi 5:00 Asubuhi. Sababu ni Kuhamisha line ya Msongo Mkubwa 11 KV ili kupisha ujenzi wa barabara wa magari yaendayo kasi  pamoja na ujenzi wa line ya kuboresha Umeme.
MAENEO YATAKAYOATHIRIKA:
Muhuto street,  Magomeni Kondoa,Mwembechai, Manzese Argentina,Kagera CCM, Manzese Sisi Kwa sisi,Manzese Midizini, Tandale Magharibi,Tandale Uzuri,Chakula bora,Manzese uzuri,Manzese Tip top, Manzese darajani,Msikiti wa Kione Manzese Kwa Mfuga Mbwa,Manzese Kanisa Katoliki,Ofisi za Kampuni ya simu, Urafiki Quarters, Millenium business, Mabibo, makuburi, mandela road, mabibo jeshini, ubungo kibangu, mabibo relini, mabibo shungashunga, ubungo maziwa,mabibo hostel, coast miller na maeneo ya jirani.
Tafadhali usishike waya uliokatika toa taarifa kupitia simu zifuatazo zifuatazo 0222171762 – 65, 0784271461, 0715271461, Au Call centre number 2194400 or 0768 985100
Uongozi unasikitika kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.
Imetolewa na:    OFISI YA UHUSIANO,
TANESCO – MAKAO MAKUU.

No comments:

Post a Comment