October 29, 2013

KATIZO LA UMEME MKOA WA MWANZA



Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linasikitika kuwataarifu wateja wake wa mkoa wa Mwanza kuwa kutakuwa na katizo la umeme siku ya ALHAMISI tarehe 31/10/2013 kuanzia saa 3.00 asubuhi hadi saa 11.00 jioni.

Sababu ni kubadilisha nguzo zilizooza na kukata matawi ya miti kwenye njia ya kusafirishia umeme kutoka kituo cha Nyakato hadi Wilaya za Nyamagana, Misungwi na Ngudu.

MAENEO YATAKAYOATHIRIKA NI:-
Ngudu Mjini, Nyambiti, Iyoma, Malya, Mwabuki, Misungwi,Ukiriguru, Usagara, Mkolani na maeneo yote ya Nyegezi.

Tafadhali usishike, usikanyage wala kusogelea nyaya za umeme zilizolala chini, toa taarifa  TANESCO Mwanza  kupitia   namba za simu zifuatazo 028 250 0090 , 028 250 1060.

Uongozi unasikitika kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.


Imetolewa na:  OFISI YA UHUSIANO
                          TANESCO -  MAKAO MAKUU.    

No comments:

Post a Comment